Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Dewji awapa ujumbe wachezaji Simba
Michezo

Dewji awapa ujumbe wachezaji Simba

Spread the love

 

SAA chache kabla ya Simba ya Dar es Salaam, kushuka dimbani kuumana na Dodoma Jiji, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa timu hiyo, Mohamed Dewji amewapa ujumbe wachezaji. Anaripoti Damas Ndembela, TUDARCo … (endelea).

Leo Ijumaa saa 10:00 jioni, katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma, Simba ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, inashuka dimbani katikamchezo wa pili wa ligi hiyo.

Mchezo wa kwanza, Simba ilitoka sare ya kutofungana na Biashara United, Uwanja wa Karume,Musoma mkoani Mara huku Dodoma Jiji yenyewe ikiiibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting, katika uwanja wake wa nyumbani.

Simba itakuwa inashuka dimbani kutafuta ushindi wa kwanza katika michezo mitatu iliyocheza pasina kushika ikitanguliwa na ule wa TP Mazembe uliomalizika kwa kipigo cha 1-0 siku ya kilele cha Simba Day na kipigo kingine cha 1-0 kutoka Yanga kwenye mechi ya Ngao ya Jamii.

Kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twitter, Dewji ambaye ni mwekezaji ndani ya timu hiyo ameweka picha akizungumza na wachezaji wa Simba na kuandika ” wachezaji wa Simba wanapaswa kukumbuka kuwa wanashikilia maisha na furaha ya watu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!