Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko DCPC: Asante Rais Samia, tulipita gizani
Habari Mchanganyiko

DCPC: Asante Rais Samia, tulipita gizani

Irene Mark Mwenyekiti DCPC
Spread the love

 

KLABU ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dara es Salaam (DCPC), kimempongeza
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuvifungulia vyombo vya habari vilivyofungiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2021, Rais Samia ameagiza wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo na wizara ya mawasiliano na teknolojia ya habari kuvifungulia vyombo vya habari vilivyofungiwa.

Vyombo hivyo ni magazeti ya MwanaHalisi, Mseto, Tanzania Daima, Mawio na Kwanza TV.

Kutokana na agizo hilo, DCPC kupitia kwa Mwenyekiti wake, Irene Mark imesema,
imefurahishwa na kauli ya Rais Samia kuwataka watendaji wa wizara hizo kuacha kutumia mabavu wakati wa kufanya uamuzi badala yake watumie kanuni na sheria zilizopo.

Samia Suluhu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

“Sisi DCPC, tunaamini watendaji wa wizara ya habari ya utamaduni, sanaa na michezo, watayafanyia kazi kwa haraka maagizo ya Rais Samia na kurejesha ajira za wanahabari na wafanyakazi wa idara nyingine zilizopotea kwa kufungwa kwa vyombo vya habari,” amesema Irene

“DCPC tunaamini kwamba, sasa uhuru wa vyombo vya habari uliominywa kwa miaka kadhaa sasa unarejea. Pia, tunaiona azma ya Rais Samia ya kuongeza mawanda ya ukusanyaji wa kodi na kusaidia katika kuleta maendeleo ya nchi.”

Irene amesema “uamuzi huu wa Rais Samia, umekuja wakati muafaka kwani tasnia ya habari kwa miaka mitano ilipita kwenye wakati mgumu hali iliyosababisha kundi kubwa la wanahabari mahiri na makini kukosa kazi.”

Pia, DCPC imetia “wito kwa wanahabari kuendelea kufanyakazi zao kwa weledi na kuzingatia sheria ya uhuru wa vyombo vya habari ya mwaka 2016 na kanuni za utangazaji ili kufanyakazi kwa amani kwa kuwa tasnia ya habari ni mhimili wa nne wa dola.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!