Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DCI, DPP kortini kwa kushindwa kuchunguza matukio ya wasiojulikana ikiwemo la Lissu
Habari za Siasa

DCI, DPP kortini kwa kushindwa kuchunguza matukio ya wasiojulikana ikiwemo la Lissu

Sylivester Mwakitalu, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP)
Spread the love

 

MWANAHABARI Luqman Maloto, amefungua kesi ya jinai dhidi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam, kwa kushindwa kuchunguza matukio yaliyofanywa na watu wasiojulikana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msajili wa mahakama hiyo tarehe 11 Januari 2023, DCI na DPP wametakiwa kufika mahakamani hapo mbele ya Jaji John Nkwabi, tarehe 8 Februari mwaka huu, kwa ajili ya usikilizaji wa kesi hiyo ya Jinai No. 5/2023.

Leo tarehe 13 Januari 2023, MwanaHALISI Online imetamfuta kwa njia ya simu Wakili anayemuwakilisha Maloto katika kesi hiyo, Hekima Mwasipu, kwa ajili ya maelezo zaidi, ambapo amejibu akisema ni kweli mteja wake amefungua kesi hiyo.

Mtandao huu umemtafuta Maloto kwa njia ya simu ili kuzungumza naye kuhusu kesi hiyo, ambaye amesema mchakato wa kuifungua kesi hiyo ulianza 2022 lakini umekamilika 2023 kwa kupangiwa tarehe na jaji.

Maloto amedai kuwa, amefungua kesi hiyo ili mahakama itamke kwamba DCI ameshindwa kufanya kazi yake ya kuchunguza matukio hayo ikiwemo tukio la Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu, kushambuliwa na risasi Septemba 2017, akiwa jijini Dodoma.

“Tunachohitaji mahakama itamke kwamba DCI na DPP hawajafanya kazi yao inavyotakiwa au wameshindwa kufanya upelelezi wa matukio hayo kuhusu kupotea au kutoweka kwa Ben Saanane, mwandishi Azory Gwanda, aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo, Simon Kanguye,”

“Tukio la Lissu kupigwa risasi na mauaji ya Akwiline Akwilini. Tunataka mahakama iseme DCI ameshindwa kufanya kazi yake ya upelekezi kuweza kusaidia Watanzania wajue nani amehusika na matukio hayo sababu ukiangalia watu ni wengi wametajwa na tumebaki dilemma hatujui kama nchi hatma ya hao watu ni nini na Watanzania tunapaswa kujua hatma yao,” amedai Maloto.

Kwa upande wa DPP, Maloto amedai kwamba “ameshindwa kwa nafasi yake kufungua mashtaka sababu angefungua tungeona kuna watu wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma za kumpiga risasi Lissu.”

Mwanahabari huyo amedai, mahakama endapo itatamka kwamba DCI na DPP wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo, hatua nyingine za kisheria zitafuatwa.

“Safari moja huwa inaanzisha nyingine, sasa tunataka mahakama isaidie kutamka kwamba wameshindwa kazi baada ya hapo hatua nyingine itafuata. Lakini tumeona tuanzie hapo mahakama inasemaje kuhusu ukimya huu, sababu tunataka tujue polisi, DCI au DPP wako kazini au wameacha,” amedai Maloto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!