SERIKALI imevifunga viwanda viwili vya wachina vilivyoko Kibaha mkoa wa Pwani vinavyojihusisha na utengenezaji wa nondo na uzalishaji wa malighafi ya kutengenezea Gypsum kutokana na kukiuka sheria na taratibu juu ya usalama mahala pa kazi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Assumpter Mshama, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha amechukua uamuzi wa kuvifunga viwanda hivyo baada kubaini ukiukwaji mkubwa wa haki za wafanyakazi ikiwemo kutowapatia wafanyakazi vitendea kazi na kuwafanyisha kazi kwa muda mrefu kitendo kinachohatarisha usalama wao.
“Sisi serikali tuko pamoja na ninyi, ndio maana tumesema hebu tumeshakuwa na viwanda sasa twende tuone watu wetu wanawatumiaje, mi nilichoona leo naomba Mamlaka ya Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) we ndio una mamlaka, wameshakufa wanne, unasikia walituambia mmoja kumbe wamekufa wanne,” amesema Mshama.
Mshama ameagiza kiwanda hicho kisifanye kazi hadi pale kitakapoweka mazingira mazuri na salama kwa wafanyakazi wake.
“Na hiki kiwanda kisifanye kazi mpaka kitakapoweka mazingira mazuri ya watu ndipo kifanye kazi, kusudi la Rais John Magufuli sio viwanda tu, ni pamoja na afya za watu, tukisema tuweke viwanda ambavyo kwenu China vimekataliwa, mfano hii mashine inayotoa moto mtu anachota na mwiko kuweka mkaa wa mawe ambao nina uhakika kwenu haumtumii kweli sisi tuko nyuma kwenye teknolojia,” amesema na kuongeza.
“Lakini huwezi kutumia mtu masaa kumi na mbili akiwa kwenye moto, lakini mawe, hizo enzi za kupiga na mkono zimepitwa na wakati. Kwa hiyo hizi sehemu mbili, uko ndani hamna shida hizo sehemu mbili hazina shida osha watakuletea barua, na mimi nitafuatilia kama mmefanyia kazi.”
Spread the love RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...
By Mwandishi WetuMarch 29, 2023Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...
By Mwandishi WetuMarch 29, 2023Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...
By Mwandishi WetuMarch 29, 2023Spread the love WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...
By Faki SosiMarch 28, 2023
Leave a comment