Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Dawasa yatangaza upungufu wa maji
Habari Mchanganyiko

Dawasa yatangaza upungufu wa maji

Bomba la maji safi
Spread the love

 

MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (Dawasa), imetangaa saa 12 za upungufu wa huduma ya maji kwa wananchi wanaohudumiwa na mtambo wa Ruvu Juu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Jamii cha Dawasa imesema, upungufu huo utatokea kwa saa 12 za leo Jumamosi tarehe 27 Machi 2021.

Sababu ya ukosefu wa majisafi ni kuruhusu, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kufanya maboresho katika laini ya umeme kutoka Chalinze.

Imeyataja maeneo yatakayoathirika ni Mlandizi, Ruvu Darajani, Vikurutu, Visiga, Misugusugu, Kongowe, Soga, Maili 35, Kwa Mfipa, Mwendapole, Kwa Mathias, Mkuza, Picha ya Ndege na Shirika la Elimu Kibaha.

Mengine ni, Pangani, Maili Moja, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Temboni, Kwa Msuguri, Saranga, Golani, Stop Over, Bonyokwa na Changanyikeni.

Pia, yamo maeneo ya Buguruni, Ubungo, Kisiwani, Msewe, Kilungule, Tabata, Segerea, Kinyerezi, Kiwalani na Pepsi mpaka Airport.

“Upatikanaji wa huduma ya maji utarejea katika hali yake ya kawaida mara tu hali ya umeme itakapotengamaa,” imeeleza Dawasa huku ikiomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!