MAMLAKA ya Maji Safi na Taka Jijini Dar es Salaam (DAWASA), imetangaza mkakati mpya wa kukarabati miundombinu yake ikiwamo mabomba yaliyotoboka, anaandika Irene David.
Hayo yamesemwa na Romanus Mwang’ingo, Kaimu Mkurugenzi Dawasa, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO), Jijini Dar es Salaam.
Amesema Dawasa imeanza kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuongeza upatikanaji wa maji, kusambaza maji katika maeneo mbalimbali, kukusanya na kusafirisha maji taka.
Mwang’ingo amesema moja ya miradi wanayotarajia kuishughulikia ni pamoja na upanuzi wa mtambo wa maji wa Ruvu chini kutoka uzalishaji wa maji mita za ujazo 180,000 hadi 270,000, ulazaji wa bomba kuu la mita 1.8 kutoka Ruvu chini hadi matenki ya chuo kikuu cha Ardhi na ujenzi wa ofisi za kuendeshea mradi huo.
Kwa upande wa mabomba yaliyotoboka kuyakarabati, Mwang’ingo amesema suala hilo lipo kwenye moja ya mikakati yao endelevu na hivyo wananchi wasihofu kwani litashughulikiwa.
Leave a comment