Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Dawasa yaibuka na mikakati lukuki Dar
Habari Mchanganyiko

Dawasa yaibuka na mikakati lukuki Dar

Spread the love

MAMLAKA ya Maji Safi na Taka Jijini Dar es Salaam (DAWASA), imetangaza mkakati mpya wa kukarabati miundombinu yake ikiwamo mabomba yaliyotoboka, anaandika Irene David.

Hayo yamesemwa na Romanus Mwang’ingo, Kaimu Mkurugenzi Dawasa, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO), Jijini Dar es Salaam.

Amesema Dawasa imeanza kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuongeza upatikanaji wa maji, kusambaza maji katika maeneo mbalimbali, kukusanya na kusafirisha maji taka.

Mwang’ingo amesema moja ya miradi wanayotarajia kuishughulikia ni pamoja na upanuzi wa mtambo wa maji wa Ruvu chini kutoka uzalishaji wa maji mita za ujazo 180,000 hadi 270,000, ulazaji wa bomba kuu la mita 1.8 kutoka Ruvu chini hadi matenki ya chuo kikuu cha Ardhi na ujenzi wa ofisi za kuendeshea mradi huo.

Kwa upande wa mabomba yaliyotoboka kuyakarabati, Mwang’ingo amesema suala hilo lipo kwenye moja ya mikakati yao endelevu na hivyo wananchi wasihofu kwani litashughulikiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!