Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawasa yaibuka na mikakati lukuki Dar
Habari Mchanganyiko

Dawasa yaibuka na mikakati lukuki Dar

Spread the love

MAMLAKA ya Maji Safi na Taka Jijini Dar es Salaam (DAWASA), imetangaza mkakati mpya wa kukarabati miundombinu yake ikiwamo mabomba yaliyotoboka, anaandika Irene David.

Hayo yamesemwa na Romanus Mwang’ingo, Kaimu Mkurugenzi Dawasa, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO), Jijini Dar es Salaam.

Amesema Dawasa imeanza kutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuongeza upatikanaji wa maji, kusambaza maji katika maeneo mbalimbali, kukusanya na kusafirisha maji taka.

Mwang’ingo amesema moja ya miradi wanayotarajia kuishughulikia ni pamoja na upanuzi wa mtambo wa maji wa Ruvu chini kutoka uzalishaji wa maji mita za ujazo 180,000 hadi 270,000, ulazaji wa bomba kuu la mita 1.8 kutoka Ruvu chini hadi matenki ya chuo kikuu cha Ardhi na ujenzi wa ofisi za kuendeshea mradi huo.

Kwa upande wa mabomba yaliyotoboka kuyakarabati, Mwang’ingo amesema suala hilo lipo kwenye moja ya mikakati yao endelevu na hivyo wananchi wasihofu kwani litashughulikiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!