Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawa za nguvu za kiume zateka Bunge
Habari Mchanganyiko

Dawa za nguvu za kiume zateka Bunge

Jengo la Bunge la Tanzania mjini Dodoma
Spread the love

MBUNGE wa Konde,Khatibu Haji (CUF) amedai kuwa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa likiwasumbua Watanzania wengi na kuihoji serikali kama kuna hatua inachukua ili kukabiliana na tatizo hilo, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali la nyongeza leo bungeni,Haji alidai kuwa tatizo hilo pia limekuwa likiwasumbua baadhi ya Wabunge kwani wamempelekea waraka (memo) wakieleza shida zao juu ya tatizo hilo.

“Mheshimiwa Spika hapa katika meza yangu nina ‘memo’ chungu nzima kutoka kwa waheshimiwa wabunge akiwemo Rashid Shangazi, Joseph Selasini, wote wakielezea shida ya jambo hili,” amesema

“Mheshimiwa Spika hivi sasa kuna utitiri wa matangazo ya biashara ya dawa za kuongeza nguvu za kiume kuna matangazo mengi yanatolewa na kusambaa nchini, jambo ambalo linaashiria ukubwa wa jambo hilo.

“Je Wizara inachukua hatua gani zinazochukuliwa kuhusu utumiaji wa dawa kiholela.

“Mheshimiwa Naibu Spika tendo la raha linahitaji furaha kuna taasisi imeeleza kuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi 10 duniani ambayo wananchi wake wamepoteza furaha.

“Sasa ni miaka 50 ya uhuru, je Serikali kwanini nchi yetu iko katika nafasi ya 10 mwisho duniani kwa kupoteza furaha mmekosea wapi,? alihoji Mbunge huyo.

Akijibu swali hilo,Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Dk.Hamisi Kigwangala alikiri Watanzania wengi kusumbuliwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!