MBUNGE wa Konde,Khatibu Haji (CUF) amedai kuwa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa likiwasumbua Watanzania wengi na kuihoji serikali kama kuna hatua inachukua ili kukabiliana na tatizo hilo, anaandika Dany Tibason.
Akiuliza swali la nyongeza leo bungeni,Haji alidai kuwa tatizo hilo pia limekuwa likiwasumbua baadhi ya Wabunge kwani wamempelekea waraka (memo) wakieleza shida zao juu ya tatizo hilo.
“Mheshimiwa Spika hapa katika meza yangu nina ‘memo’ chungu nzima kutoka kwa waheshimiwa wabunge akiwemo Rashid Shangazi, Joseph Selasini, wote wakielezea shida ya jambo hili,” amesema
“Mheshimiwa Spika hivi sasa kuna utitiri wa matangazo ya biashara ya dawa za kuongeza nguvu za kiume kuna matangazo mengi yanatolewa na kusambaa nchini, jambo ambalo linaashiria ukubwa wa jambo hilo.
“Je Wizara inachukua hatua gani zinazochukuliwa kuhusu utumiaji wa dawa kiholela.
“Mheshimiwa Naibu Spika tendo la raha linahitaji furaha kuna taasisi imeeleza kuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi 10 duniani ambayo wananchi wake wamepoteza furaha.
“Sasa ni miaka 50 ya uhuru, je Serikali kwanini nchi yetu iko katika nafasi ya 10 mwisho duniani kwa kupoteza furaha mmekosea wapi,? alihoji Mbunge huyo.
Akijibu swali hilo,Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Dk.Hamisi Kigwangala alikiri Watanzania wengi kusumbuliwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.
Leave a comment