Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko DART yabadili ratiba ya mabasi
Habari Mchanganyiko

DART yabadili ratiba ya mabasi

Spread the love

KUFUATIA ujenzi wa daraja la juu kwenye makutano ya barabara ya Morogoro na Mandela, Kampuni ya UDA Rapid Transport (UDART)  inayotoa huduma kwenye mfumo wa mabasi yaendayo haraka imetangaza kubadili ratiba ya huduma zake. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa UDART, Deus Bugaywa amesema mabadiliko hayo yataanza 30 Julai, 2018 ambapo asubuhi mabasi yanayotoa huduma ya Express kutoka Ubungo- Kivukoni na namba 005 ya Ubungo- Gerezani yataanzia safari zake katika kituo cha Ubungo Terminal badala ya Ubungo Maji.

Bugaywa amesema wakati wa mchana na jioni mabasi hayo yataendelea na huduma zake kama kawaida zisizokuwa Express badala ya kuishia Ubungo Maji sasa yataishia Ubungo Terminal.

“Kutokana na mabadiliko haya tunawashauri abiria wetu waliokuwa wakitumia kituo cha Ubungo Maji hasa nyakati za asubuhi watumie zaidi kituo vha Ubungo Terminal,” amesema.

Hata hivyo amesema wakati ujenzi huo ukiendelea mabasi ya mwendo wa haraka yatatumia njia moja tu (Single lane) ambapo ndio sababu kubwa ya mabasi hayo kuishia Terminal kwa lengo la kupunguza msongamano katika kituo wakati wa kushusha abiria hivyo UDART inaomba radhi abiria wake kwa usumbufu huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!