KUFUATIA ujenzi wa daraja la juu kwenye makutano ya barabara ya Morogoro na Mandela, Kampuni ya UDA Rapid Transport (UDART) inayotoa huduma kwenye mfumo wa mabasi yaendayo haraka imetangaza kubadili ratiba ya huduma zake. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa UDART, Deus Bugaywa amesema mabadiliko hayo yataanza 30 Julai, 2018 ambapo asubuhi mabasi yanayotoa huduma ya Express kutoka Ubungo- Kivukoni na namba 005 ya Ubungo- Gerezani yataanzia safari zake katika kituo cha Ubungo Terminal badala ya Ubungo Maji.
Bugaywa amesema wakati wa mchana na jioni mabasi hayo yataendelea na huduma zake kama kawaida zisizokuwa Express badala ya kuishia Ubungo Maji sasa yataishia Ubungo Terminal.
“Kutokana na mabadiliko haya tunawashauri abiria wetu waliokuwa wakitumia kituo cha Ubungo Maji hasa nyakati za asubuhi watumie zaidi kituo vha Ubungo Terminal,” amesema.
Hata hivyo amesema wakati ujenzi huo ukiendelea mabasi ya mwendo wa haraka yatatumia njia moja tu (Single lane) ambapo ndio sababu kubwa ya mabasi hayo kuishia Terminal kwa lengo la kupunguza msongamano katika kituo wakati wa kushusha abiria hivyo UDART inaomba radhi abiria wake kwa usumbufu huo.
Leave a comment