MATOKEO ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) 2022 yanaonesha kuwa ufaulu wa watahiniwa katika masomo yote uko juu ya wastani isipokuwa kwa somo la Kiingereza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa tathmini ya awali ya matokeo hayo yaliyotangazwa leo tarehe 1 Disemba, 2022 na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), kwa upande wa somo la hilo la Kiingereza jumla ya watahiniwa 59,990 (4.45%) wamepata Daraja la A.
Watahiniwa 56,569 (4.20%) wamepata Daraja la B, watahiniwa 279,580 (20.74%) wamepata Daraja la C, watahiniwa 912,708 (67.71%) wamepata Daraja la D wakati waliopata Daraja la E ni 39,086 sawa na asilimia 2.90.
Aidha, takwimu za somo la Hisabati zinaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 43,362 (3.22%) wamepata Daraja la A, watahiniwa 133,288 (9.89%) wamepata Daraja la B, watahiniwa 541,623 (40.18%) wamepata Daraja la C, watahiniwa 613,442 (45.51%) wamepata Daraja la D na waliopata Daraja la E ni 16,267 sawa na asilimia 1.21.
Somo la Sayansi na Teknolojia jumla ya watahiniwa 67,071 (4.98%) wamepata Daraja la A, watahiniwa 287,690 (21.34%) wamepata Daraja la B, watahiniwa 610,839 (45.31%) wamepata Daraja la C, watahiniwa 360,031 (26.71%) wamepata Daraja la D na waliopata Daraja la E ni 22,362 sawa na asilimia 1.66.
Leave a comment