Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko CWT yalalamikia Wilaya Chamwino kunyanysa walimu
Habari Mchanganyiko

CWT yalalamikia Wilaya Chamwino kunyanysa walimu

Spread the love

CHAMA cha Walimu Chamwino mkoani Dodoma (CWT) kimelalamikia walimu kufanyishwa kazi siku za mapumziko ya mwisho wa wiki bila malipo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Pia kimeeleza kuwa, walimu hao hawapewi chakula kinyume na kanuni na miongozo ya kazi kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini.

Malalamiko hayo yametolewa leo tarehe 18 Februari 2019 na Clement Mahemba, Mwenyekiti wa CWT wilaya hiyo wakati alipozungumza na waandishi wa habari wilayani hapo.

Mahemba amedai, utaratibu huo ambao umeandaliwa na Ofisa Elimu Msingi wilayani hapo umekuwa ukinyanyasa walimu kutokana na kuwatumikisha siku za mapumziko ambazo ni Jumamosi na Jumapili.

Amedai, pamoja na walimu hao kutumikishwa kazi katika siku za kwenda kufanya ibada lakini pia katika mpango huo ambao ofisa elimu huyo anauita kuwa ni vikao kazi, kumekuwa hakuna malipo yoyote wala chakula.

“Walimu wanafanyishwa kazi siku za Jumamosi pamoja na Jumapili siku ambazo wengi wao wanatakiwa kufanya mapumziko kwa jili ya kujiandaa Jumatatu kwenda kufundisha,” amesema na kuongeza;

“Lakini pia walimu hawa wanatoka umbali mrefu kuna walimu wanatoka Kijiji cha Champumba kwenda Mlowa barabarani ni zaidi ya kilomita 80 kwenda kushiriki vikao kazi hivyo n ahata kukosa muda wa kufanya maandalizi ya Jumatatu.”

Mahemba amesema, kitendo cha mwajiri kumwita mtumishi wake kazini siku za mapumziko anatakiwa kumlipa kama ambavyo sheria ya ajira na mahusiano kazini namba 6 ya mwaka 2004 kifungu cha 24(1)6 na 24(4) vinavyoelekeza.

Akijibu malalamiko hayo Athumani Massasi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chamwino amesema, anachofahamu ni kuwa, hakuna mwalimu aliyelazimishwa na kwamba, wote wanafanya hivyo kwa utayari wao.

“Ninacho kifahamu mimi mwandishi, hawa walimu ni makubalianao yao hivyo hakuna mwalimu yeyote ambaye amelazimishwa kufanya hivyo wanavyofanya sasa lakini kama unataka kufahamu zaidi njoo ofisini,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!