Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CUF Z’bar washtukia faulo uchaguzi 2020
Habari za SiasaTangulizi

CUF Z’bar washtukia faulo uchaguzi 2020

Spread the love

MBUNGE wa Malindi Visiwani Zanzibar, Ali Salehe (CUF) amedai kuwa, kuna mkakati wa kuzuia baadhi ya wananchi katika kujiandikisha kwenye usajili wa vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Salehe alitoa madai hayo jana tarehe 4 Oktoba 2018 wakati akizungumza na wanahabari, ambapo aliihusisha hatua hiyo na mkakati wa kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Alidai kuwa, kitendo hicho ni miongoni mwa figisu zinazoandaliwa na wanasiasa na kuitaka serikali kuingilia kati suala hilo.

Wakizungumza katika nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa jimbo hilo, walidai kuwa, wamekuwa wakikumbana na masharti magumu pindi wanapokwenda kujisajili huku baadhi yao wakieleza kuwa, baadhi ya wahusika wamekuwa wakihitaji kiasi cha fedha ndipo wafanye usajili.

Akizungumzia kuhusu sakata hilo, Dk. Hussein Shabaan, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Usajili wa Matokeo ya Kijamii Zanzibar, alilaani figisu hizo akisema kila Mzanzibar mwenye sifa stahiki anatakiwa kupata kitambulisho, na kuwataka wahusika kutoa kitambulisho hicho pasina ubaguzi.

Dk. Shaaban alisisitiza kuwa, ili mwananchi apate kitambulisho anatakiwa kuwa na cheti cha kuzaliwa pamoja na barua kutoka kwa sheha wa shehia husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!