MOHAMED Faki, mgombea udiwani katika Kata ya Vingunguti (CUF) Dar es Salaam ameanza kukaangwa mapema. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Mawakala wa Faki wamezuiwa kuingia kwenye vyumba vya kupigia kura Jambo linalomwacha mdomo wazi.
Mawakala wake watano amesema wamekataliwa kuingia kumsaidia kusimamia kura zake katika Kituo cha Upigaji Kura Cha Shule ya Msingi Miembeni kwa madai hawatambuliki.
“Mawakala wangu wanazo fomu na wakiwaonesha wanasema sio pale lakini zinaonesha Ni kituo hicho,” amesema Faki.
Na kwamba hana cha kufanya kwa kuwa, kwenye kituo hicho tayari amepigwa bao mapema.
Leave a comment