Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CUF wacharuka kufukuzwa Wenyeviti wake
Habari za Siasa

CUF wacharuka kufukuzwa Wenyeviti wake

Spread the love

UONGOZI wa Chama cha Wananchi CUF wameanza kutafuta mwarobaini wa kuwarejesha wenyeviti sita wa Wilaya ya Chemba, Dodoma pamoja na mikoa mingine walioondolewa kwa amri ya wakuu wa wilaya. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Uongozi huo ukiongozwa na Mratibu wa Makamu Mwenyekiti CUF Tanzania Bara, Rajabu Mbalamwezi ambaye alifanya kikao na wananchi wa wilaya hiyo alisema kitendo kilichofanywa na mkuu wa Wilaya Chemba, Salmon Odunga pamoja na wakuu wengine wa wilaya ni makosa kisheria. 

Mbalamwezi katika kikao hicho amesema CUF kwa sasa imetangaza kuwarejesha wenyeviti wote wa vijiji walioondolewa kwa amri ya wakuu wa wilaya.

“Wakuu wa wilaya wamekuwa wakiitisha mkutano wa hadhara na kutengeneza makosa feki na kuwaondoa wenyeviti wa Miranda sasa CUF imetangaza kuwarejesha wote walioondolewa na hilo ni nchi nzima.

“Haiwezekani Mkuu wa wilaya anaamka na maamuzi yake na ikumbukwe kuwa hao wenyeviti wamepigiwa kura wamechaguliwa na wananchi kwa hali hiyo wenyeviti wanatakiwa kuheshimiwa,” amesema Mbalamwezi.

Hivi  karibuni wakuu wa wilaya walikuwa wakitumia mikutano kwa kuwasimamisha wenyeviti wa vijiji ambao wanatokana na vyama vya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!