Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF wacharuka kufukuzwa Wenyeviti wake
Habari za Siasa

CUF wacharuka kufukuzwa Wenyeviti wake

Spread the love

UONGOZI wa Chama cha Wananchi CUF wameanza kutafuta mwarobaini wa kuwarejesha wenyeviti sita wa Wilaya ya Chemba, Dodoma pamoja na mikoa mingine walioondolewa kwa amri ya wakuu wa wilaya. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Uongozi huo ukiongozwa na Mratibu wa Makamu Mwenyekiti CUF Tanzania Bara, Rajabu Mbalamwezi ambaye alifanya kikao na wananchi wa wilaya hiyo alisema kitendo kilichofanywa na mkuu wa Wilaya Chemba, Salmon Odunga pamoja na wakuu wengine wa wilaya ni makosa kisheria. 

Mbalamwezi katika kikao hicho amesema CUF kwa sasa imetangaza kuwarejesha wenyeviti wote wa vijiji walioondolewa kwa amri ya wakuu wa wilaya.

“Wakuu wa wilaya wamekuwa wakiitisha mkutano wa hadhara na kutengeneza makosa feki na kuwaondoa wenyeviti wa Miranda sasa CUF imetangaza kuwarejesha wote walioondolewa na hilo ni nchi nzima.

“Haiwezekani Mkuu wa wilaya anaamka na maamuzi yake na ikumbukwe kuwa hao wenyeviti wamepigiwa kura wamechaguliwa na wananchi kwa hali hiyo wenyeviti wanatakiwa kuheshimiwa,” amesema Mbalamwezi.

Hivi  karibuni wakuu wa wilaya walikuwa wakitumia mikutano kwa kuwasimamisha wenyeviti wa vijiji ambao wanatokana na vyama vya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!