Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF kumkabidhi Rais Samia ilani zake
Habari za Siasa

CUF kumkabidhi Rais Samia ilani zake

Mhandisi Mohammed Ngulangwa, Mkurugenzi wa Habari -CUF
Spread the love

 

CHAMA cha Wananchi (CUF), kimesema kitamkabidhi ilani za chama hicho kuanzia Uchaguzi Mkuu wa 1995 hadi 2020 pindi ombo lao la kukutana naye litakapotekelezwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Ombi hilo limetolewa na Mhandisi Mohammed Ngulangwa, Mkurugenzi wa Habari CUF wakati akizungumza na MwanaHALISI Online kuhusu siku 100 za Rais Samia madarakani.

“Tunamuomba afungue milango ya mashauriano na viongozi wa vyama, awe tayari kupokea ilani za uchaguzi mfululizo za CUF.  Tangu tumeanza mfumo wa vyama vingi, yapo mengi atajifunza na kumfanya awe rais wa mfano,” amesema Ngulangwa.

Rais Samia aliyeingia madarakani tarehe 19 Machi 2021, kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli, kilichotokea tarehe 17 Machi mwaka huu.

Kiongozi huyo wa awamu ya sita wa Tanzania, anafikisha siku 100 keso tarehe 27 Juni 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!