Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo Cristiano Ronaldo ruksa kuivaa Man United
Michezo

Cristiano Ronaldo ruksa kuivaa Man United

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA) limethibitisha kumfungia mchezo mmoja wa Ligi ya Mabingwa mshambuliaji wa klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo baada ya kuoneshewa kadi nyekundu kwenye mchezo dhidi ya Valencia. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Baada ya UEFA kutengua kadi hiyo mshambuliaji huyo ataukosa mchezo mmoja tu dhidi ya Young Boys Jumanne 2 Oktoba 2018 na hivyo atakuwa tayari kuivaa Manchester United katika mchezo wa klabu bingwa unaotarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Old Trafford Oktoba, 2018.

Ronaldo alipewa kadi hiyo baada ya kumvuta nywele mlinzi wa klabu ya Valencia, Jeison Murillo alipokuwa akimkaba na muamuzi kuamua kumchukulia hatua hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!