Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Cristiano Ronaldo arejea Man U
Michezo

Cristiano Ronaldo arejea Man U

Spread the love

 

BAADA ya kuondoka ndani ya Manchester United ya Uingereza miaka 12 iliyopita, Cristiano Ronaldo (36) ametangazwa kurejea tena ndani ya timu akitokea Juventus ya Italia. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea). 

Ronaldo maarufu kama CR7 raia wa Ureno, ametangazwa kurejea viunga vya Old Trafford, alipoondoka mwaka 2009 kwenda kujiunga na vigogo wa Hispania timu ya Real Madrid.

Ronaldo ambaye ameshinda mataji zaidi ya 30, alijiunga na Real Madrid akitokea Manchester United kwa pauni milioni 80 mwaka 2009 na kufunga jumla ya mabao 451 inaelezwa.

Mitandao mbalimbali ya Man U, jioni ya leo Ijumaa tarehe 27 Agosti 2021, imemtambulisha mchezaji bora mara tano wa dunia ‘Ballon d’Or’ mwaka 2008, 2013, 2014, 2016 na 2017 na kuandika maneno “karibu nyumbani.”

CR7 alikuwa akihusishwa na kutua Man City au PSG ya Ufaransa lakini amekijuta akirejea sehemu alipopata mafanikio makubwa.

Kocha wa Juventus, Massimiliano Allegri alinukuliwa akieleza Ronaldo akimweleza hana mpango tena wa kuwachezea mabingwa hao wa Italia.

Ronaldo alisajiliwa na Manchester United kwa dau la la £12.2m mwaka 2003 akitokea Sporting Lisbon ya Ureno na kufanikiwa kufunga magoli 118 katika mechi 292 akiichezea.

Alihudumu Real Madrid toka mwaka 2009 hadi Julai 2018 alipotangazwa kutimkia Italia na kujiunga na Juventus ambayo hadi anaondoka, ameiwezesha timu hiyo kutwaa mataji mbalimbali ikiwemo la ligi kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!