Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa COVID-19: Magogo ya kuchomea watu India yaadimika
Kimataifa

COVID-19: Magogo ya kuchomea watu India yaadimika

Spread the love

 

IDADI kubwa ya vifo vinavyotokana na virusi vya corona (COVID – 19), nchini India, imesababisha uhaba wa magogo ya kuchomea watu. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Taarifa zinaeleza, India inataabika na uhaba wa magogo kwa kuwa, idadi ya watu wanaokufa na kuhitaji huduma hiyo kulingana na Imani yao, imekuwa kubwa nchini humo.

India kwa sasa ndio nchi namba moja kuwahi kutokea katika kurekodi idadi kubwa ya maambukizi ndani ya siku moja na ongezeko la kasi la vifo.

Tofauti na nchi zilizowahi kushika nafasi za juu katika kurekodi maambukizi mapya – Marekani, Brazil na Mexico – sasa India inarekodi zaidi ya watu 300,000 kwa siku huku idadi ya vifo ikiongezeka.

Katika Mji Mkuu wa nchi hiyo – Delhi, eneo la maegesho ya magari limegeuzwa na kuwa sehemu ya kuchomea watu wanaofariki dunia kulingana na Imani yao.

Idadi kubwa wagonja nchini humo wanataabika na kupata huduma ya mtungi wa gesi ya oksijeni ili kuwasaidia kupumua. Kwa sasa India tatizo si kuwa na pesa ya kupata huduma hiyo, bali upatikanaji wa huduma hiyo. kili

Kwa siku saba mfululizo, India imerekodi zaidi ya maambukizi 300,000 kwa siku, hali inayotishia usalama wa taifa hilo lililo na watu bilioni 1.4.

Jumapili wiki iliyopita, Waziri wa Afya wa India, Dk. Harsh Vardhan alieleza taifa hilo kurekodi maambukizi mapya 360,960 katika saa 24 na kuweka rekodi ya kuwa na maambukizi milioni 18 katika taifa hilo. Siku hiyo waliofariki dunia ni 3,293.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!