Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya COVID-19: Askofu Gwajima aonya serikali
Afya

COVID-19: Askofu Gwajima aonya serikali

Askofu Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe
Spread the love

 

ASKOFU Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ametoa tahadhari kwa serikali juu ya chanjo ya virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akichangiwa wakati wa mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka 2021/22, Askofu Gwajima amesema, Taifa linatakiwa kuchukua tahadhari kabla ya kuruhusu chanjo ya corona kwa wananchi.

Amesema, hapingani na chanjo ya corona, lakini amesisitiza umakini katika aina ya chanja iwapo Tanzania itataka kuridhia.

Kwamba, kumekuwa na ‘chanjo mwendo kasi,’ ambapo inapohojiwa sababu ya haraka hiyo, “najibiwa kwa sababu teknolojia imekuwa.”

Askofu Gwajima amesema, chanzo za sasa zimechukua muda mchache kulinganisha na chanjo nyingine miaka ya nyuma, kwamba zilichukua mpaka miaka 10 kabla ya kuingizwa sokoni.

Amesema, chanzo zinazotumika sasa, zimeruhusiwa na mamlaka ya dharura ambao wanadai, madhara yanayotokana katika chanjo ni kutokana na mtumiaji mwenyewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!