MSANII wa Bongofleva, Rajabu Abdul maarufu kama Harmonize au Kondeboy amewaomba radhi mashabiki wake baada ya kubadili ratiba ya ‘tour’ (ziara) yake kwenye baadhi ya nchi za bara la Ulaya na Amerika Kaskazini kutokana na masharti ya virusi vya Corona. Anaripoti Matilda Buguye, Dar es Salaam … (endelea).
Harmonize ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram mapema leo tarehe 22 Septemba 2021, akiwa huko jijini Las vegas nchini Marekani.
Aidha, CEO huyo wa lebo ya Konde Music World Wide anaendelea na tour yake kwenye baadhi ya maeneo nchini humo.
Msanii huyo amesema, “watu wangu wa Canada na Sweden naomba radhi kwa kuwa nimeshindwa kukamilisha ratiba ya tarehe tuliyoipanga kwa sababu ya vizuizi vya Uviko 19″
Hata hivyo, msanii huyo amesema atatoa tarehe mpya hivi karibuni kwa wale mashabiki wake ambao tayari walishakata tiketi kwe ajili ya kwenda kuwapa burudani kama ilivyopangwa.
Pia Harmonize ametangaza kuendelea na tour yake kwenye maeneo yaliyobakia ambayo hayana vizuizi vya Uviko 19.
Kwa mujibu wa ratiba yake, tarehe 23 Septemba atakuwa Las Vegas, Oktoba mosi – New York, Tarehe 9 Oktoba – Los Angels, 15 Oktoba- Idaho, 22 Oktoba – Minnesota na 23, Oktoba – Suracus New York.
Hadi sasa ameshakamua katika majimbo ya Ohio, Huston Texas, Pheonix, na Los vegas na mengine.
Leave a comment