Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona yaitesa Afrika: Congo, Rwanda, Zimbabwe hakutoshi
Afya

Corona yaitesa Afrika: Congo, Rwanda, Zimbabwe hakutoshi

Dk. John Nkengasong, Mkurugenzi wa Kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika (CDC)
Spread the love

GONJWA hatari la Corona, sasa limerejea kwa kasi katika Bara la Afrika, ambako mamilioni ya watu tayari wameambukizwa ugonjwa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam  … (endelea).

Wimbi hili la pili la Corona linalokumba Afrika ni “kali zaidi” kuliko la kwanza, kwa mujibu wa Dk. John Nkengasong wa Kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika (CDC).

Nkengasong ameliambia shirika la habari la BBC kwamba, bara hilo kwa sasa, linaripoti maambukizi mapya ya karibu 30,000 kila siku ikilinganishwa na 18,000 katikati ya mwezi Julai.

Takwimu za shirika hilo la afya zinaonesha kwamba Afrika kufikia sasa imethibitisha kuwa watu karibu milioni 3 wameambukizwa virusi vya corona, na vifo 68,755.

Nchi kama Rwanda, Namibia, Zimbabwe na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimeweka vikwazo vipya vya kuzuia kuenea kwa virusi.

 

Dk. Nkengasong alisema kuvaa barakoa ndio njia pekee ya kuzuia kuenea kwa virusi na kutoa wito kwa serikali kupunguza bei ya bidhaa hiyo.

Aliongeza kusema: “Unapotembea katika nchi tofauti barani Afrika inasikitisha kuona watu wengi hawavai barakoa mara kwa mara ama hawavai kabisa, na pia hawazingatii umati kati ya mtu moja na mwingine. Hii ni hatari, wimbi la pili ni kali sana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!