SERIKALI ya Kenya imeripoti wagonjwa wapya 149 wa virusi vya corona (COVID-19) baada ya kupima sampuli 3,090 ndani ya saa 24 zilizopita. Anaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea)
Maambukizo yamefikia 5,533 na vifo vimeongezeka na kufikia 137 baada ya wagonjwa watano kufariki dunia.
Wagonjwa 48 wameruhusiwa kutoka Hospitalini na kufanya idadi ya waliopona ugonjwa huo kufika 1,905.
Kenya imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kila siku za corona ambapo leo Ijumaa tarehe 26 Juni 2020, naibu waziri wa afya wan chi hiyo, Dk. Rashid Aman kati ya wagonjwahao 149 wapya, 148 ni Wakenya na mmoja ni raia wa kigeni.
Amesema, wanaume ni 94 na wanawake ni 55 wenye umri kati ya miaka 76.
Dk. Aman amesema, kati ya wagonjwa hao 149; Nairobi (73), Mombasa (20), Kajiado (15), Siaya (13), Machakos (3), Kilifi (1), Nakuru (1), Nandi (1), Bungoma (1), Isiolo (1).
Leave a comment