Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Corona yaendelea kuitesa Kenya, vifo vyafikia 137
Kimataifa

Corona yaendelea kuitesa Kenya, vifo vyafikia 137

Spread the love

SERIKALI ya Kenya imeripoti wagonjwa wapya 149 wa virusi vya corona (COVID-19) baada ya kupima sampuli 3,090 ndani ya saa 24 zilizopita. Anaripoti Mitandao ya Kimataifa  … (endelea)

Maambukizo yamefikia 5,533 na vifo vimeongezeka na kufikia 137 baada ya wagonjwa watano kufariki dunia.

Wagonjwa 48 wameruhusiwa kutoka Hospitalini na kufanya idadi ya waliopona ugonjwa huo kufika 1,905.

Kenya imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kila siku za corona ambapo leo Ijumaa tarehe 26 Juni 2020, naibu waziri wa afya wan chi hiyo, Dk. Rashid Aman kati ya wagonjwahao 149 wapya, 148 ni Wakenya na mmoja ni raia wa kigeni.

Amesema, wanaume ni 94 na wanawake ni 55 wenye umri kati ya miaka 76.

Dk. Aman amesema, kati ya wagonjwa hao 149; Nairobi (73), Mombasa (20), Kajiado (15), Siaya (13), Machakos (3), Kilifi (1), Nakuru (1), Nandi (1), Bungoma (1), Isiolo (1).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!