Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona yaanza kulipuka upya Hong Kong
Afya

Corona yaanza kulipuka upya Hong Kong

Spread the love

MJI wa Hong Kong nchini China, leo Jumatano tarehe 13 Mei 2020, umeripoti wagonjwa wawili wapya wenye maambukizo wa virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti Aljazeera…(endelea).

Mamlaka za jiji hilo zimeeleza, maambukizi hayo ni ya ndani (local transition), na yamethibitisha kwamba watu hao walioambukizwa, hawajakutana na watu wowote kutoka nje ya taifa ama jiji hilo.

Hatua hiyo imeshtua mamlaka za jiji hilo hasa kutokana na waathirika hao kutokuwa karibu ama kukutana na watu kutoka nje ya jiji ama taifa hilo.

Mamlaka za jiji hilo sasa zinaamini, maambukizo bado yapo mtaani ikiwa ni wiki moja baada ya kufungua shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na majumba ya sinema, majumba ya mazoezi na sehemu za vilevi (bar).

Kutokana na mafanikio ya awali, mamlaka za jiji hilo zilieleza mpango wake mpya wa kufungua shule mwishoni mwa mwezi huu wa Mei.

Hata hivyo, sasa zinafikiria upya. Zuio la kundi la watu wanaoanzia wanane, lipo palepale.

Jiji hilo ambalo ni muhimu kwa uchumi Asia na duniani kote, ni miongoni mwa majiji yaliyofanikiwa kwa kiwango kikubwa kudhibiti ugonjwa huo pale ulipoanza kulipuka.

Ni jiji ambalo katika hatua za mwanzo kabisa, liliwaweka watu wake karantini na kutumia njia mbalimbali wanavikabili virusi hivyo ikiwa ni pamoja na sheria zingine zilizowekwa ili kufikia lengo.

Hata hivyo, taarifa ya kuwepo kwa maambukizi hayo, hasa tabu ya kufuatilia namna walivyopata maambukizi hayo watu hao, kumewaweka kwenye tahadhari kubwa kwamba, huenda mazingira yajayo yakawa magumu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!