SHIRIKA la Afya Duniani (WHO), limetoa tahadhari kwa dawa za mitishamba zinazotengenezwa ili kukabiliana na virusi vinavyosababisha homa ya mapafu (corona). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
WHO imetoa taarifa hiyo wakati ambao baadhi ya mataifa ya Afrika yakijielekeza nchini Madagascar kuchukua dawa iliyotengenezwa kwa mitishamba.
Shirika hilo limeeleza, kwamba ni vizuri dawa ni muhimu dawa zinazosemekana kuwa na uwezo wa kutibu, kufanyiwa majaribio kwanza.
“…huenda watu wakaona wamepata tiba na kujihisi kuwa salama, ikiwa watakuwa na imani na dawa ambazo hazijafanyiwa majaribio,” wameeleza.
Miongoni mwa nchi zilizoeleza wazi kutumia dawa iliyopatikana nchini Madagascar ni Tanzania, Jamuhuri ya Congo, Guinea Bissau na Equatorial Guinea.
Mataifa haya, yameeleza wazi kwamba watatuma ndege nchini Madagascar kuchukua dawa hiyo ya mitishamba.
Dawa hiyo inayohusishwa na mmea wa Kichina unaoitwa Artemisia (pakanga), mmea huo ni mojawapo ya miti ambayo huchanganywa pamoja na mimea mingine ya Madagascar kama tiba ya ugonjwa wa Malaria.
Leave a comment