Saturday , 9 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Corona: Rais wa Brazil ‘sijambo,’ Hong Kong yafunga shule
Habari Mchanganyiko

Corona: Rais wa Brazil ‘sijambo,’ Hong Kong yafunga shule

Spread the love

JAIR Bolsonaro, Rais wa Brazil amewaambia wananchi wake, kwamba anaendelea vizuri ikiwa ni siku chache baada ya kutangaza kuambukizwa virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Jumanne wiki hii baada ya kufanyiwa vipimo, Bolsonaro alitangaza kwamba amebainika kuwa na virusi vya corona. Na kwamba, aliamua kufanya vipimo kwa kuwa alikuwa na joto kali pamoja na kikohozi.

“Nipo vizuri” Bolsonaro ameandika ujumbe huo kwenye ukurasa wake wa Facebook akisisitiza kwamba, amekuwa akitumia dawa aina ya Chloroquine ambayo haijathibitishwa na wanasayansi.

Matumizi ya Chloroquine katika kupambana na COVID-19, yaliyoanza kupigiwa chapuo na Donald Trump, Rais wa Marekani na baadaye Bolsonaro, yanapingwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), kwamba hakuna ushahidi kuwa dawa hiyo inaponesha.

Katika Jiji la Hong Kong, China hali ya maambukizi ya COVID-19 inatishia amani ambapo serikali ya jiji hilo, imetangaza kufunga shule zote.

Maambukizi mapya 42 yaliyoripotiwa kwenye jiji hilo Jumanne wiki hii, imesukuma utawala kufunga shule hizo ili kuzuia maambukizi zaidi. Shule hizo zimetakiwa kufungwa kuanzia Jumatatu wiki ijayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

Habari Mchanganyiko

Tanesco: Mvua chanzo kukatika umeme leo

Spread the loveShirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limedai kuwa hitilafu iliyojitokeza katika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Zara tours yajivunia kupandisha wageni 228 Mlima Kilimanjaro

Spread the loveKampuni ya utalii ya Zara tours ya mjini Moshi mkoani...

error: Content is protected !!