Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Corona: Rais wa Brazil ‘sijambo,’ Hong Kong yafunga shule
Habari Mchanganyiko

Corona: Rais wa Brazil ‘sijambo,’ Hong Kong yafunga shule

Spread the love

JAIR Bolsonaro, Rais wa Brazil amewaambia wananchi wake, kwamba anaendelea vizuri ikiwa ni siku chache baada ya kutangaza kuambukizwa virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Jumanne wiki hii baada ya kufanyiwa vipimo, Bolsonaro alitangaza kwamba amebainika kuwa na virusi vya corona. Na kwamba, aliamua kufanya vipimo kwa kuwa alikuwa na joto kali pamoja na kikohozi.

“Nipo vizuri” Bolsonaro ameandika ujumbe huo kwenye ukurasa wake wa Facebook akisisitiza kwamba, amekuwa akitumia dawa aina ya Chloroquine ambayo haijathibitishwa na wanasayansi.

Matumizi ya Chloroquine katika kupambana na COVID-19, yaliyoanza kupigiwa chapuo na Donald Trump, Rais wa Marekani na baadaye Bolsonaro, yanapingwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), kwamba hakuna ushahidi kuwa dawa hiyo inaponesha.

Katika Jiji la Hong Kong, China hali ya maambukizi ya COVID-19 inatishia amani ambapo serikali ya jiji hilo, imetangaza kufunga shule zote.

Maambukizi mapya 42 yaliyoripotiwa kwenye jiji hilo Jumanne wiki hii, imesukuma utawala kufunga shule hizo ili kuzuia maambukizi zaidi. Shule hizo zimetakiwa kufungwa kuanzia Jumatatu wiki ijayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!