Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Corona janga la dharura – WHO
Kimataifa

Corona janga la dharura – WHO

Spread the love

TEDROS Adhanom, Kiongozi Mkuu wa Shirika la Afya duniani (WHO), ametangaza kwamba virusi vya Corona sasa ni janga la dharura duniani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Adhanom amesema “watu takribani 213 wamefariki kutokana na virusi hivyo nchini China.”

Amesema, WHO limedhibitisha, kwamba kumekuwa na visa 98 katika mataifa mengine 18 ingawa hakuna vifo virivyoripotiwa. Visa vingi vya wagonjwa hao vilitokana na watu waliosafiri kutoka mji wa Wuhan, China eneo ambalo mlipuko wa ugonjwa huo ulipoanzia.

“Sababu kubwa ya tangazo hilo si kwa sababu ya kile ambacho kinatokea China kwa sasa, lakini kile ambacho kinatokea katika mataifa mengine,” amesema Adhanom.

Hata hivyo, Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya nchini Tanzania amesema, mtu yeyote atakayepata virusi vya Corona ndani ya Tanzania, atatibiwa katika maeneo yaliyotengwa yaliyopo mkoani Kilimanjaro, Dar es Salaam na Mwanza na kwamba, mpaka sasa hakuna mkasa wa virusi hivyo nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!