MAAMBUKIZO ya virusi vya corona (COVID-19) duniani, yamefikia milioni 21.8, waliopona milioni 14.5 huku waliofariki dunia kutokana na ugonjwa huo wakiwa 773,122. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Mtandao wa worldometer leo Jumatatu tarehe 17 Agosti 2020 unaonyesha, Marekani inaongoza kwa kuwa na maambukizo milioni 5.5, waliofariki 173,128 na waliopona milioni 2.9.
Brazili ni taifa la pili dunia likiwa na maambukizo milioni 3, waliopona milioni 2.4 na waliofariki dunia 107,879.
China ambako COVID-19 ilianzia mwishoni mwa mwaka 2019, ni taifa la 33 duniani ikiwa na maambukizo 84,849 kati ya hao, waliopona ni 79,603 na waliofariki dunia wakiwa 4,634.
Leave a comment