Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Coco beach kuboreshwa, Bakhresa kupeleka boti za utalii
Habari Mchanganyiko

Coco beach kuboreshwa, Bakhresa kupeleka boti za utalii

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla amesema, amepata wadau waliokubali kuwajengea wafanyabiashara wa ufukwe wa Coco vibanda vya kisasa na kuboresha mandhari ya ufukwe huo ili uwe kwenye mwonekano wa kisasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

RC Makalla amesema hayo leo Jumanne, tarehe 24 Agosti 2021, alipotembelea ufukwe huo akiambatana na viongozi na wadau waliokubali kuwa sehemu ya maboresho ya fukwe wakiwemo Bank za NMB, CRDB, Kampuni za utengenezaji wa Vinywaji zikiwemo TBL, Coca-Cola, Pepsi, Asas na Azam group.

Amesema wa dhamira yake na Serikali ni kuona Coco inakuwa ya kisasa na shughuli za kiutalii zinafanyika ambapo tayari amezungumza na Mfanyabiashara mkubwa nchini Said Salim Bakhresa kwaajili ya kuleta boti za utalii kwenye fukwe hiyo.

Aidha RC Makalla ameelekeza Manispaa ya Kinondoni kuanza mara moja Ujenzi wa Ofisi, Stoo na vyoo vya kisasa kwenye ufukwe huo.

Hata hivyo, Makalla ametoa maelekezo kwa Manispaa ya Kinondoni kupeleka umeme eneo lote la Coco huku akimuelekeza Kamanda wa Polisi Kinondoni kuimarisha ulinzi kwenye ufukwe huo.

Mpango wa RC Makalla kuboresha fukwe za Dar es Salaam unaenda sambamba na maboresho ya maeneo ya wazi, ustani za kupumzika, usafi na upandaji wa miti, maua na kinbgo pembezoni mwa Barabara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!