Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Chuo cha Mati Ilonga kusaidia vijana kujikwamua kiuchumi
Habari Mchanganyiko

Chuo cha Mati Ilonga kusaidia vijana kujikwamua kiuchumi

Spread the love

VIJANA nchini wametakiwa kukitumia vyema Chuo cha Kilimo – Mati Ilonga ili kupata elimu mbalimbali ikiwemo ya usindikaji wa mazao itakayowasaidia kujikwamua kiuchumi sambamba na kufikia uchumi wa viwanda. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Dk. Mdangi Mashaka amesema hayo kwenye maonesho ya wakulima 88 kanda ya Mashariki wakati akiongea na waandishi wa Habari ndani ya viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere eneo la Tungi nje kidogo ya Manispaa ya Morogoro.

Dk. Mashaka alisema, chuo hicho kilichopo wilayani Kilosa mkoani hapa kina uwezo wa kutoa elimu za usindikaji na uzalishaji wa mazao mbalimbali kama vile mazao ya mikunde, mbegu, mbogamboga na mizizi kinauwezo wa kupokea wanafunzi 180 kwa mwaka lakini kinapokea wanafunzi wasiofika 100 na kufanya elimu inayotolewa kutofika vyema kwa jamii.

Alisema, kufuatia elimu hiyo vijana wanaweza kufikia hatua ya kujiajiri katika kukuza uchumi wa viwanda na hivyo kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 kama ulivyo mpango wa Serikali.

Naye Mkuu wa Idara ya Elimu ya Ushauri kwa wakulima kutoka Mati-Ilonga, John Ngairo alisema, elimu inayotolewa katika chuo hicho huweza kuwasaidia wakulima kuongeza mnyororo wa thamani na kuweza kuuza kwa bei kubwa na yenye faida.

Hivyo aliwashauri vijana na wakulima kwa ujumla kwenda kwenye chuo hicho kujifunza namna ya kuongeza mnyororo wa thamani na hivyo kuondokana na umaskini wa kipato kufuatia kuwa na ujuzi wa kuweza hata kuanzisha viwanda vidogovidogo.

“usindikaji wa mazao hauhitaji vitu vingi na haugharimu fedha nyingi bali ni elimu tu ambayo mkulima akiamua kuielewa naweza anzisha na kujikwamua kiuchumi” alisema.

Naye Mkufunzi kutoka Chuo hicho, Hamisi Ramadhani alisema, usindikaji una faida mbalimbali kwa mkulima na hata kwa mtumiaji wa bidhaa za usindikaji kwani bidhaa hizo huongezewa thamani na hivyo kuwa na vitamin, protin na madini yanayoweza kulinda afya ya mlaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!