KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Danieli Chongolo, amewatahadharisha wanachama wa chama hicho ambao walipata dhamana ya uongozi wa Serikali za Mitaa lakini hawatimizi majukumu yao na kusababisha wananchi kuichukia. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).
Chongolo ametoa tahadhari hiyo leo Jumanne tarehe 24 Januari, 2023, wakati wa kuitambulisha Sekretarieti kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyofanyika makao makuu ya CCM Jijini Dodoma.
Chongolo amewataka kila mmoja atimize wajibu wake ili kuepukana na chuki hiyo ambayo inaweza kuwasababishia wananchi kuwauliza maswali mengi wakati wa kuendelea kutafuta dola na kushika dola.
“Chama chochote cha siasa kazi yake kutafuta na kushika dola sasa tuna kazi ya kusimamamia dola tuliyopewa na dhamana ya kuishika na wananchi ili ifikapo 2025 tusiende kuulizwa maswali na wananchi,” amesema Chongolo.
“Ndugu zangu 2019 chama kilipewa dhamani ya kushika nafasi za serikali za mitaa wajibu huo unatakiwa kuusimamia ili tuendelee kuaminiwa zaidi na zaidi ndugu zangu wajibu huo si wakukaa, kilegelege, wala kuzembea;
“Mkoa badala ya kutimiza wajibu wake anakaa analalamika hayupo kwenye wajibu wa kusikiliza malalamiko ya watu bali yupo kwenye kulaumu, utamkuta Waziri aliyepewa wajibu na majukumu ya kufanya kazi na kupewa dhanana ya kuwatumikia watu anashindwa kutumikia badala yake anachelewesha maendeleo,” amesema Chongolo.
Aidha Chongolo amewakemea baadhi ya viongozi ndani ya serikali kwa kuendeleza malalamiko badala ya kufanya kazi kwa kutimiza majukumu yao.
Mbali na kuwakemea Viongozi hao amewatangazia kihama viongozi hao ambao wanatumia muda mwingi kulalamika na kwamba kulalamika kwao kunaonesha wazi kuwa hawatoshi.
Leave a comment