Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chongolo alia na vigingi misamaha ya kodi miradi ya kimkakati
Habari za Siasa

Chongolo alia na vigingi misamaha ya kodi miradi ya kimkakati

Spread the love

 

KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, amesema vigingi vilivyowekwa kwenye misamaha ya kodi ndio kikwazo kikubwa kinachosababisha kuchelewa kukamilika kwa wakati baadhi ya miradi ya maendeleo na kimkakati inayoendelea kutekelezwa hapa nchini. Anaripoti Christina Haule, Kilombero … (endelea).

Amesema kutokana na changamoto hiyo, ipo haja ya kuwepo kwa dirisha moja ambalo litakuwa linawajibika na miradi inayoingia nchini ambayo inahitaji kutekelezwa kupitia msamaha wa kodi, hiyo ni baada ya kushindwa kukamilika kwa wakati ujenzi wa daraja la Ruaha Mkuu linalounganisha Mikumi na Kilombero kutokana na vikwazo vya msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani VAT.

Chongolo ametoa kauli hiyo wakati akiwa Ifakara, wilayani Kilombero mkoani Morogoro ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku tisa inayolenga kukagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 pamoja na kuzungumza na makundi mbali mbali ya kijamii.

“Serikali ni moja, msamaha wa kodi tunatoa wenyewe, mradi tuna sainisha wenyewe, halafu jambo moja la msamaha wa kodi linakuwa nyuma wakati la kusaini mradi linakuwa mbele, ninadhani ifike mwisho na isiwe hoja tena kwa wananchi” amesema Chongolo.

Chongolo ameongeza kuwa kuanzia sasa Serikali inapaswa kuweka mfumo wa kuhakikisha msamaha wa kodi hauwi kikwazo tena kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

“Mpaka inaitwa msamaha wa kodi maana yake ndani ya Serikali kumechakatwa mradi, tukakubaliana kwamba mradi utatekelezwa kwa kuondosha kodi na hasa ya Ongezeko la Thamani, kwa hiyo lazima twende tukashughulike na hilo” amesisitiza Chongolo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!