KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Daniel Chongolo amekemea tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali kupanga watumishi wa umma kwenye vituo vya kazi vya mjini kwa upendeleo wa kujuana na kuwapangia wengine vituo vya vijijini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu … (endelea).
Kauli hiyo ameitoa leo Ijumaa tarehe 3 Juni, 2022 wilayani Busega katika Kata ya Mkula Mkoa wa Simiyu akihitimisha ziara yake mkoani humo ya kukagua uhai wa chama kwenye mashina na utekelezaji wa ilani kwenye miradi ya maendeleo.
Akikagua ujenzi wa kituo cha afya cha Mkula, kilichokamilika ujenzi wake uliogharimu Sh.400 milioni na kinachotarajiwa kuanza kutoa huduma tarehe 20 Juni 2022, Katibu Mkuu amekemea tabia ya kupanga watumishi katika vituo vya kazi kwa upendeleo.
“Tuache upendeleo wa kupanga watumishi wa umma, baadhi ya watendaji mnapanga kwa kuwalundika eneo moja la mjini kwa kuangalia kujuana, wengine mnawapanga vijijini, ni vyema mkawapanga kwa kuangalia mahitaji ya eneo kwa sababu vituo vyote vya kazi vinahudumia wananchi na wote wanahitaji huduma,”amesema Chongolo.
Asante ndugu chongolo lakini uwelewo kuwa upendeleo upo ngazi zote ktk taifa letu wengine wamepewa vio vikubwa kwa upendeleo nawala hawatimizi wajibu