ASKARI Mpelelezi wa Polisi nchini Tanzania, H4347 Goodluck, ambaye ni shahidi wa pili wa jamhuri katika kesi ndogo ndani ya kesi ya uhujumu uchumi, inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, amehojiwa iwapo amepandishwa cheo kutokana na kushiriki tukio la kuwakamata watuhumiwa wawili wa kesi hiyo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelsa).
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala amemuuliza swali hilo leo Jumanne, tarehe 23 Novemba 2021, katika mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mawasiliano jijini Dar es Salaam, mbele ya Jaji Joachim Tiganga.
Ni baada ya shahidi huyo kuieleza mahakama hiyo namna alivyoshiriki kuwakamata washtakiwa wawili katika kesi hiyo, Adam Kasekwa na Mohammed Abdillah Ling’wenya, tarehe 5 Agosti 2020, maeneo ya Rau Madukani mkoani Kilimanjaro.
Mahojiano yao yalikuwa hivi;
Kibatala: Nimesikia una cheo tofauti na ulichokuwa nacho wakati unawakamata watuhumiwa wawili?
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Umeshuka au umepanda?
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Nitakuwa sahihi nikisema baada ya matukio haya yamekupandisha cheo?
Shahidi: Sio sahihi, elimu yangu imenipandisha cheo, na sio baada ya kazi niliyofanya ndiyo nimepanda cheo.
Kibatala: In terms of time cheo kimekuja baada ya kufanya kazi hiyo?
Shahidi: Siyo sahihi, imekuja kutokana na elimu yangu
Kibatala: Ni sahihi tukio lilianza na kikafuta cheo?
Shahidi: Sio sahihi, sababu nimepa kwa sababu ya elimu yangu
Jaji Tiganga: swali lake ni baada?
Shahidi: Hapana
Kibalata: Ulipanda cheo tarehe ngapi?
Shahidi: Nilipanda cheo tarehe 23 Agosti 2021
Kibatala: Na ilikuwa kabla?
Shahidi: Bada ya kukamata watuhumiwa
Kibatala: Baada ya kupanda cheo cha awali na mmeibua nyie wenyewe, Wakili Hilla alikuongoza kufafanua namna ulivyopanda cheo labda kutokana na elimu yako, alikuongoza kufafanua?
Shahidi: Hapana
Kibatala alimuuliza swali hilo baada ya askari huyo wakati akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Pius Hilla, alipodai kuwa alipandishwa cheo tarehe 23 Agosti 2021.
Goodluck alidai yeye ni askari polisi tangu 2013 alipoajiriwa na Jeshi la Polisi, na kwamba anafanya kazi katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha, Idara ya Upelezi wa Makosa ya Jinai.
Wakili Hilla alimuongiza shahidi huyo kama ifuatavyo;
Hilla: Sasa hivi una cheo gani
Shahidi: Hivi sasa ni Sergent
Hilla: Ulikioata lini?
Shahidi: Nilikipata tarehe 23 Agosti 2021
Hilla: 2020 ulikuwa na cheo gani?
Shahidi: Polisi Constable/Detective
Hilla: Vipo daraja gani?
Shahidi: Idara ya Upelelezi Makosa ya Jinai
Hilla: Ni muda gani uko kwenye hiyo idara?
Shahidi: Nina muda wa miaka mitatu
Hilla: Majukumu yako ni nini?
Shahidi: Majukumu yangu ni kukamata wahalifu, kufanya upelelezi, kukusanyavielelezo na kitekeleza majukumu mbalimbali ninayopewa na viongozi wangu.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu kujua undani wa kesi hiyo ambayo shahidi anaendelea kutoa ushahidi wake
Asante sana kwa habari iliyopangwa vizuri. Asante kwa kuandika majibizano halisi ya sehemu ya kupandishwa cheo kwa shahidi.
Rafiki yako,
Aliko Musa.
Real Estate Consultant