Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Michezo Chelsea, Man City kushuka dimbani leo
Michezo

Chelsea, Man City kushuka dimbani leo

Sergio Aguero, Mshambuliaji wa Manchester City
Spread the love

LIGI Kuu nchini Uingereza kuendelea tena hii leo, ambapo klabu ya Manchester City itashuka dimbani kuwakabili Everton, huku Chelsea ikiwa nyumbani itapata wakati wa kujiuliza mbele ya Astorn Villa mara baada ya kupoteza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Arsenal. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Chelsea walipoteza mchezo huo kwa mabao 3-1 mbele ya Arsenal ambao hawakupata ushindi katika michezo saba iliyopita ya Ligi Kuu toka walivyowafunga Manchester United Novemba Mosi, 2020.

Mpaka sasa Ligi hiyo imeshachezwa michezo 15 kwa baadhi ya timu, huku Liverpool akiendelea kuwa kileleni mwa msimamo ikiwa na pointi 32 licha ya kubanwa mbavu na West Brom kwenye mchezo wa jana, nafasi ya pili ikishikwa na Everton akiwa na pointi 29 na nafasi ya tatu wakiwa Leicester City wenye pointi 28.

Mchezo mwengine utakuwa ni Crystal Palace ambao watakuwa nyumbani kuwakabili Leicester City na siku ya kesho tarehe 29 Desemba, 2020, Arsenal watakuwa ugenini dhidi ya Brighton, huku Manchester United ikiwaalika Wolves.

Ligi hiyo itaendelea tena siku ya Jumatano tarehe 30 Desemba, 2020 kwa michezo miwili ambapo Tottenham baada ya kulazimishwa sare dhidi ya Wolves ya bao 1-1, wataialika Fulham na vinara wa Ligi hiyo ambao pia ni mabingwa watetezi klabu ya Liverpool watakuwa ugenini kuwakabili Newcastle United.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!