NAIBU Rais wa Kenya, William Ruto amefanya mkutano na maofisa wapya wa ulinzi kutoka kitengo cha utawala nchini humo ambao amepewa na serikali. Anaripoti mwandishi Wetu … (endelea).
Kwenye video ambazo amepakia mitandaoni, Ruto anaonekana akiwa matembezeni na maofisa hao katika makazi yake kabla ya kuketi na kunywa chai pamoja nao.
“Nanywa chai na walinzi wangu wapya, nawakaribisha katika makazi yangu rasmi,” Ruto alisema.
Awali iliripotiwa kuwa Serikali ya Kenya ilimpokonywa Ruto walinzi ambao walikuwa maofisa wa kitengo cha kitengo cha huduma ya jumla (GSU) waliokuwa wakilinda makazi yake yaliyoko Mtaan Karen na Sugoi.
Maofisa hao waliondolewa siku ya Alhamis, Agosti 26, hatua iliyomfanya Ruto kulalamikia usalama wake.
Msemaji wa Ruto, David Mugonyi alisema mabadiliko hayo yalifanywa bila mazungumzo wala makubaliano yoyote.
Mugoyi alisema kamanda wa polisi wa Mtaani Karen alipewa amri kutoka ofisi kuu ikimuagiza kuwaondoa maofisa hao haraka kabla ya muda wa adhuhuri.
Ruto pia amedai kwamba wapinzani wake wanafanya kila wawezalo kuhakikisha wanakamdamiza kabisa kisiasa.
Awali, mfanyakazi wake mkuu Ken Osinde alikuwa amelalamika kwamba walinzi wa Ruto walikuwa wamepunguzwa bila serikali kutoa taarifa yoyote.
Maofisa hao waliondolewa katika kipindi ambacho tofauti baina ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake zimeonekana hadharani hali ambayo imemfanya Rais kumtaka naibu wake kujiuzulu kama amechoka.
Leave a comment