Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Cheki Naibu Rais alivyowakaribisha walinzi wapya… wanywa chai pamoja
Kimataifa

Cheki Naibu Rais alivyowakaribisha walinzi wapya… wanywa chai pamoja

Spread the love

 

NAIBU Rais wa Kenya, William Ruto amefanya mkutano na maofisa wapya wa ulinzi kutoka kitengo cha utawala nchini humo ambao amepewa na serikali. Anaripoti mwandishi Wetu … (endelea).

Kwenye video ambazo amepakia mitandaoni, Ruto anaonekana akiwa matembezeni na maofisa hao katika makazi yake kabla ya kuketi na kunywa chai pamoja nao.

“Nanywa chai na walinzi wangu wapya, nawakaribisha katika makazi yangu rasmi,” Ruto alisema.

Awali iliripotiwa kuwa Serikali ya Kenya ilimpokonywa Ruto walinzi ambao walikuwa maofisa wa kitengo cha kitengo cha huduma ya jumla (GSU) waliokuwa wakilinda makazi yake yaliyoko Mtaan Karen na Sugoi.

Maofisa hao waliondolewa siku ya Alhamis, Agosti 26, hatua iliyomfanya Ruto kulalamikia usalama wake.

Msemaji wa Ruto, David Mugonyi alisema mabadiliko hayo yalifanywa bila mazungumzo wala makubaliano yoyote.

Mugoyi alisema kamanda wa polisi wa Mtaani Karen alipewa amri kutoka ofisi kuu ikimuagiza kuwaondoa maofisa hao haraka kabla ya muda wa adhuhuri.

Ruto pia amedai kwamba wapinzani wake wanafanya kila wawezalo kuhakikisha wanakamdamiza kabisa kisiasa.

Awali, mfanyakazi wake mkuu Ken Osinde alikuwa amelalamika kwamba walinzi wa Ruto walikuwa wamepunguzwa bila serikali kutoa taarifa yoyote.

Maofisa hao waliondolewa katika kipindi ambacho tofauti baina ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake zimeonekana hadharani hali ambayo imemfanya Rais kumtaka naibu wake kujiuzulu kama amechoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!