UWANJA wa mpira wa Chato, Geita ambao utatumika katika shughuli ya kuaga mwili ya Hayati John Magufuli, upo kwenye maandalizi. Anaripoti Tunu Herman, Chato … (endelea).
Rais Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Mchi 2021, jijini Dar es Salaam kwa ugionjwa wa moyo.
Serikali wilayani Chato inatumia magreda pamoja na vifaa mbalimbali vya kisasa, kuhakikisha maandalizi hayo yanakamilika haraka.
Mwandishi wetu aliyepo Chato, anaeleza kutawala kwa utulivu huku mijadala ya hapa na pale ikiendelea kuhusu kifo cha Rais Magufuli.
Tayari uwanja huo umebadilika mandhari yake na kuwa ya kuvutia.
Morine Tambwe, mmoja wa wakazi wa Chato anasema, wilaya hiyo imeumizwa na kifo hicho.
“Hapa tumeumia zaidi kwa kuwa, ndio kiongozi pekee aliyeiweka Chato kwenye taswira ya Tanzania na kujulikana,” amesema.
Amesema, vijana wa Chato walikuwa na matumaini makubwa kuendelea kubaki ndani ya wilaya hiyo kutokana mabadiliko yaliyodhihirika kwa kasi ya pekee.
“Tunaamini viongozi wanaomfuata, hawataitelekeza Chato na maeneo mengine,” amesema.
Leave a comment