Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Chato maandalizi ya kumuaga JPM yashika kasi
Habari Mchanganyiko

Chato maandalizi ya kumuaga JPM yashika kasi

Spread the love

 

UWANJA wa mpira wa Chato, Geita ambao utatumika katika shughuli ya kuaga mwili ya Hayati John Magufuli, upo kwenye maandalizi. Anaripoti Tunu Herman, Chato … (endelea).

Rais Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Mchi 2021, jijini Dar es Salaam kwa ugionjwa wa moyo.

Serikali wilayani Chato inatumia magreda pamoja na vifaa mbalimbali vya kisasa, kuhakikisha maandalizi hayo yanakamilika haraka.

Mwandishi wetu aliyepo Chato, anaeleza kutawala kwa utulivu huku mijadala ya hapa na pale ikiendelea kuhusu kifo cha Rais Magufuli.

Tayari uwanja huo umebadilika mandhari yake na kuwa ya kuvutia.

Morine Tambwe, mmoja wa wakazi wa Chato anasema, wilaya hiyo imeumizwa na kifo hicho.

“Hapa tumeumia zaidi kwa kuwa, ndio kiongozi pekee aliyeiweka Chato kwenye taswira ya Tanzania na kujulikana,” amesema.

Amesema, vijana wa Chato walikuwa na matumaini makubwa kuendelea kubaki ndani ya wilaya hiyo kutokana mabadiliko yaliyodhihirika kwa kasi ya pekee.

“Tunaamini viongozi wanaomfuata, hawataitelekeza Chato na maeneo mengine,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!