Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Chato maandalizi ya kumuaga JPM yashika kasi
Habari Mchanganyiko

Chato maandalizi ya kumuaga JPM yashika kasi

Spread the love

 

UWANJA wa mpira wa Chato, Geita ambao utatumika katika shughuli ya kuaga mwili ya Hayati John Magufuli, upo kwenye maandalizi. Anaripoti Tunu Herman, Chato … (endelea).

Rais Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Mchi 2021, jijini Dar es Salaam kwa ugionjwa wa moyo.

Serikali wilayani Chato inatumia magreda pamoja na vifaa mbalimbali vya kisasa, kuhakikisha maandalizi hayo yanakamilika haraka.

Mwandishi wetu aliyepo Chato, anaeleza kutawala kwa utulivu huku mijadala ya hapa na pale ikiendelea kuhusu kifo cha Rais Magufuli.

Tayari uwanja huo umebadilika mandhari yake na kuwa ya kuvutia.

Morine Tambwe, mmoja wa wakazi wa Chato anasema, wilaya hiyo imeumizwa na kifo hicho.

“Hapa tumeumia zaidi kwa kuwa, ndio kiongozi pekee aliyeiweka Chato kwenye taswira ya Tanzania na kujulikana,” amesema.

Amesema, vijana wa Chato walikuwa na matumaini makubwa kuendelea kubaki ndani ya wilaya hiyo kutokana mabadiliko yaliyodhihirika kwa kasi ya pekee.

“Tunaamini viongozi wanaomfuata, hawataitelekeza Chato na maeneo mengine,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!