Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Chanjo yaua 15 Sudan Kusini
Kimataifa

Chanjo yaua 15 Sudan Kusini

Watoto Sudan Kusini
Spread the love

SERIKALI ya Sudan kusini imesema watoto wapatao 15 wamekufa ikiwa ni matokeo ya makosa yaliyofanyika katika jaribio la kuwakinga na surua, anaandika Hamisi Mguta.

Wafanyakazi wa afya katika jimbo la mashariki Ikweta walirudia tena kutumia sindano zisizo na usafi kuwachanja watoto wote.

Waziri wa Afya wa Sudan kusini Riek Gai Kok amesema timu iliyohusika katika kampeni hiyo ya chanjo haikuwa na vigezo wala kupata mafunzo kwa kazi hiyo.

Hata hivyo, huduma za afya zimekuwa zikifanya kazi kwa shida Sudan kusini toka kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

error: Content is protected !!