Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Chanjo ya corona yawaponza 2 Arusha, wasimamishwa
Tangulizi

Chanjo ya corona yawaponza 2 Arusha, wasimamishwa

Ummy Mwalimu
Spread the love

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Ummy Mwalimu, ameagiza kuchukuliwa hatua watumishi wawili wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Mwalimu Omary Kwesiga, Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi na Scolastica Kanje, Afisa Muuguzi Msaizidi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Ni baada ya watumishi hao, Mwalimu Kwesiga na Kanje ambaye anafanya kazi Hospitali ya Mkoa ya Arusha kufanya igizo kwenye shughuli ya chanjo ya corona, kinyume cha taratibu na kanuni za utoaji wa chanjo.

Kitendo hicho kimeleta sintofahamu kwa wananchi kuhusu zoezi la chanjo linaloendelea nchini nzima baada ya kuzinduliwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, tarehe 28 Julai 2021, Ikulu ya Dar es Salaam.

Taarifa ya Nteghenjwa Hoseah, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Tamisemi, aliyoitoa leo Ijumaa tarehe 6 Agosti 2021 imesema, Waziri Ummy “amemuagiza Katibu Mkuu Tamisemi kumsimamisha kazi Mwalimu Kwesiga na Scolastica apelekwe kwenye baraza la wauguzi na wakunga kwa hatua zaidi.”

Katika kipande cha video cha sekundi 37 kinachosambaa mitandaoni, kinaonyesha jinsi muuguzi huyo, Scolastica akijaribisha kuchoma chanjo ya corona Mwalimu Kwesiga huku kiuhalisi hakufanya hivyo.

Tayari Agnes Mtawa, Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, amemuagiza muunguzi wa mkoa wa Arusha ambaye ni msimamizi wa taaluma katika mkoa, kumsimamisha kazi miezi mitatu, Scolastica “kisha kutoa taarifa ya zoezi zima lililopelekea muuguzi huyo kufanya kitendo hicho.”

Agnes kupitia taarifa yake kwa umma amewaasa wauguzi na wakunga kuzingatia viapo kwa kutia huduma kwa weledi na kuzingatia maadili ya taaluma ili kuepusha usumbufu kwa wananchi usiokuwa wa lazima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za SiasaTangulizi

Makonda awapopoa wanaomtofautisha Magufuli na Samia

Spread the loveKATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),...

error: Content is protected !!