Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Chanjo ya corona: WHO yaitenga Tanzania, Burundi
Afya

Chanjo ya corona: WHO yaitenga Tanzania, Burundi

Spread the love

 

SHIRIKA la Afya duniani (WHO), limeiondoa Tanzania na Burundi katika orodha ya nchi za Afrika Mashariki zikazopewa chanjo ya virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti BBC…(endelea).

Taarifa zinaeleza, chanjo (dozi) milioni 336 za AstraZeneca/Oxford na Pfizer-BioNTech, zitatolewa kwa muhula wa kwanza na wa pili wa mwaka 2021.

Nchi ambazo zitanufaika na chanjo hiyo ni Kenya (dozi 4,176,000), Rwanda (dozi 1,098,960), Sudan Kusini (dozi 864,000) na Uganda (dozi) 3,552,000. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ipo kwenye orodha hiyo.
WHO limetangaza mpango wa muda kuhusu na namna nchi hizo zitakavyopatiwa ili kujikinga na maambukizi ya corona.

Kwa awamu hii, nchi hizo zitapatiwa chanjo kwa idadi ya asilimia ya watu 3.3 kwa kila nchi, ni kutokana na malengo ya shirikisho la chanjo duniani (GAVI), ya utoaji wa chanjo kwa asilimia tatu ya wakazi dunia ndani ya miezi sita ya kwanza ya mwaka 2021.

Mataifa mengine ambayo hayatopewa chanji na WHO ni Equatorial Guinea, Eritrea, Gabon, Lesotho, Madagascar na Ushelisheli.

Wiki iliyopita Rais wa Tanzania, John Magufuli aliitahadharisha Wizara ya Afya kutopokea chanjo za corona, aliitaka wizara hiyo kuwa makini.

WHO imeeleza sababu ya kutojumuisha nchi hizo kwenye mpango wake wa chanjo ni kutokana na zilijinunulia chanjo zake zenyewe na hazikuomba au hazimo katika orodha ya nchi zitakazopewa chanjo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!