Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Maisha Afya Chanjo ya corona: WHO yaitenga Tanzania, Burundi
Afya

Chanjo ya corona: WHO yaitenga Tanzania, Burundi

Spread the love

 

SHIRIKA la Afya duniani (WHO), limeiondoa Tanzania na Burundi katika orodha ya nchi za Afrika Mashariki zikazopewa chanjo ya virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti BBC…(endelea).

Taarifa zinaeleza, chanjo (dozi) milioni 336 za AstraZeneca/Oxford na Pfizer-BioNTech, zitatolewa kwa muhula wa kwanza na wa pili wa mwaka 2021.

Nchi ambazo zitanufaika na chanjo hiyo ni Kenya (dozi 4,176,000), Rwanda (dozi 1,098,960), Sudan Kusini (dozi 864,000) na Uganda (dozi) 3,552,000. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ipo kwenye orodha hiyo.
WHO limetangaza mpango wa muda kuhusu na namna nchi hizo zitakavyopatiwa ili kujikinga na maambukizi ya corona.

Kwa awamu hii, nchi hizo zitapatiwa chanjo kwa idadi ya asilimia ya watu 3.3 kwa kila nchi, ni kutokana na malengo ya shirikisho la chanjo duniani (GAVI), ya utoaji wa chanjo kwa asilimia tatu ya wakazi dunia ndani ya miezi sita ya kwanza ya mwaka 2021.

Mataifa mengine ambayo hayatopewa chanji na WHO ni Equatorial Guinea, Eritrea, Gabon, Lesotho, Madagascar na Ushelisheli.

Wiki iliyopita Rais wa Tanzania, John Magufuli aliitahadharisha Wizara ya Afya kutopokea chanjo za corona, aliitaka wizara hiyo kuwa makini.

WHO imeeleza sababu ya kutojumuisha nchi hizo kwenye mpango wake wa chanjo ni kutokana na zilijinunulia chanjo zake zenyewe na hazikuomba au hazimo katika orodha ya nchi zitakazopewa chanjo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

Afya

LHRC yapinga kufutwa Toto Afya: Ni ukiukaji wa sheria za watoto

Spread the love  KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimekosoa...

Afya

Manesi 7 mbaroni tuhuma za kuwauzia dawa wagonjwa usiku wa manane

Spread the love  JUMLA ya wauguzi/manesi saba wa Hospitali ya Manispaa ya...

error: Content is protected !!