Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Chanjo Covid-19 yaingia rasmi Tanzania, wananchi waitwa
AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo Covid-19 yaingia rasmi Tanzania, wananchi waitwa

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesema chanjo ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19), imeshaingia nchini. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 21 Julai 2021 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza katika swala ya Eid El-Adha, iliyofanyika kwenye Msikiti wa Mtoro, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

“Chanjo ipo anayetaka akanchanje hospitalini,  zimeelezwa mahali zilipo nenda ili utimize haja yako lakini pia ni kinga, wenzetu wanachanja kama kinga,” amesema Waziri Majaliwa.

Waziri mkuu huyo wa Tanzania, amesema chanjo hiyo imeingizwa baada ya watalaamu wa afya kuzifanyia uchambuzi na kubaini kwamba hazina madhara.

“Madaktari wawaliagizwa wafanye utafiti wa chanjo nzuri ambazo watu wametumia hawajapata madhara, tukawaambia fanyeni uchunguzi katika chanjo zote duniani. Kwetu tumepata chache, aina mbili tatu tukasema tuzilete nchini, anayetaka achanje,” amesema Waziri Majaliwa.

Amesema Serikali imeamua kuingiza chanjo hizo, ili kuwaondolea usumbufu wananchi hasa wanaofanya shughuli zao nje ya nchi.

“Serikali ilikaa chini na kutafakari na kugundua kuwa Watanzania wengi ambao wanashughuli mbalimbali, ikiwemo wanaotaka kwenda hija yenye masharti ya kwenda ukiwa umechanjwa na kuna Watanzania wanafanyabiashara nje ya nchi wanataka watu wawe wamechanjwa,” amesema Waziri Majaliwa.

Waziri Majaliwa ameongeza “Rais Samia Suluhu Hassan,   akasema hebu tukae pamoja tutafakari hili jambo hao Watanzania wanaotaka kwenda kwenye maeno haya watatimizaje masharti hayo, maamuzi yakafikiwa walete chanjo kadhaa,” amesema Waziri Majaliwa.

Waziri Majsliwa amewataka Watanzania wazidi kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Covid-19, akisema kuwa nchi ina wagonjwa kadhaa wa ugonjwa huo.

Amewataka Watanzania kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, kuvaa barako pamoja na kunawa mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!