Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Michezo Chama uso kwa uso na Simba, kombe la Shirikisho
Michezo

Chama uso kwa uso na Simba, kombe la Shirikisho

Spread the love

 

Clatous Chama Raia wa Zambia akiwa na kikosi cha RS Berkane atakutana uso kwa uso na timu yake ya Zamani ya Simba kwenye mchezo ya hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho Barani Afrika kufuatia kupangwa kundi moja. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Timu hizo mbili zimepangwa kundi D, sambamba na Asec Mimosa kutoka Ivory Coast na US Gendarmerie Nationale ya Nigeria mara baada ya kuchezeshwa droo hii leo.

Chama anakutana tena na waajili wake wa zamani ikiwa imepita miezi mine toka alipoachana nao na kujiunga na RS Berkane ya nchini Morocco kwenye dirisha kubwa la usajili sambamba na winga wa klabu ya Yanga, Tuisila Kisinda.

Mchezaji huyo aliondoka ndani ya klabu ya Simba huku akiwa na m,afanikio makubwa ikiwa kuipeleka timu hiyo hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya Mabingwa mara mbili na kutwaa mataji matatu ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ikumbukwe RS Berkane kwa sasa inanolewa na Florence Ibenge kocha wa zamani wa klabu ya AS Vita ya nchini Congo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!