CHAMA kipya cha siasa nchini Tanzania kinachojinasibisha na ‘Rais wa Wanyonge’, John Magufuli, kimeanza kuleta sintofahamu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya baadhi ya viongozi wake, wakiwamo wabunge na waliokuwa mawaziri, kuhusishwa nacho. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Taarifa ndani ya chama tawala-CCM zinasema, hofu ya baadhi ya viongozi kuhusu ujio wa chama hicho kipya cha Umma Party (UP), ni kutokana na hofu kuwa baadhi ya wanaokiunga mkono, ni waliokuwa wasaidizi wa karibu na Rais Magufuli.
Umma Party kilizinduliwa juzi Jumapili, Manzese, jijini Dar es Salaam, huku viongozi wake wakiwa wamevalia fulana zenye picha ya Rais Magufuli, huku kwenye mitandao ya kijamii, mjadala mkubwa ukiwa ni uundwaji wa chama hicho.
Haya yanatokea, zikiwa zimesalia takribani miaka mitatu kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani, huku chama hicho kikiendelea kutafuta wadhamini ili kupata usajili wa kudumu.
Taarifa zinahusishwa na chama hicho na minong’ono kuwa miongoni mwa waasisi wake, ni vigogo walioko CCM na Upinzani.
Undani wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema la leo Jumanne tarehe 19 Aprili 2022 kujua alichosema mwenyekiti wake, Seif Maalim Seif na mengine mengi.
Leave a comment