Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Chama ‘Magufuli’ moto, mawaziri nawabunge wahusishwa kujiunga
HabariTangulizi

Chama ‘Magufuli’ moto, mawaziri nawabunge wahusishwa kujiunga

Spread the love

 

CHAMA kipya cha siasa nchini Tanzania kinachojinasibisha na ‘Rais wa Wanyonge’, John Magufuli, kimeanza kuleta sintofahamu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya baadhi ya viongozi wake, wakiwamo wabunge na waliokuwa mawaziri, kuhusishwa nacho. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa ndani ya chama tawala-CCM zinasema, hofu ya baadhi ya viongozi kuhusu ujio wa chama hicho kipya cha Umma Party (UP), ni kutokana na hofu kuwa baadhi ya wanaokiunga mkono, ni waliokuwa wasaidizi wa karibu na Rais Magufuli.

Umma Party kilizinduliwa juzi Jumapili, Manzese, jijini Dar es Salaam, huku viongozi wake wakiwa wamevalia fulana zenye picha ya Rais Magufuli, huku kwenye mitandao ya kijamii, mjadala mkubwa ukiwa ni uundwaji wa chama hicho.

Haya yanatokea, zikiwa zimesalia takribani miaka mitatu kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani, huku chama hicho kikiendelea kutafuta wadhamini ili kupata usajili wa kudumu.

Taarifa zinahusishwa na chama hicho na minong’ono kuwa miongoni mwa waasisi wake, ni vigogo walioko CCM na Upinzani.

Undani wa habari hii, soma Gazeti la Raia Mwema la leo Jumanne tarehe 19 Aprili 2022 kujua alichosema mwenyekiti wake, Seif Maalim Seif na mengine mengi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!