Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Michezo Chama, Kagere, Niyonzima Carlinhos waikosa Yanga vs Simba  
Michezo

Chama, Kagere, Niyonzima Carlinhos waikosa Yanga vs Simba  

Clatous Chama
Spread the love

MABINGWA watetesi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba imesema katika mchezo wa kesho Jumamosi dhidi ya watani zao Yanga watakosa huduma ya kiungo wao, wao Clatous Chama, Bernard Morrison na Meddy Kagere. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea) 

Chama aliumia katika mchezo uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) 2020/21 uliochezwa Jumatano ya tarehe 4 Novemba 2020 dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, Simba iliibuka na ushindi wa 2-0. Magoli hayo yalifungwa na nahodha John Bocco kwa penati na Hamis Ndemla aliyepokea pasi ya Chama.

Chama ambaye ni raia wa Zambia hakumaliza mchezo huo baada ya kuumia kwenye mchezo huo na kutoka dakika ya 69 na nafasi yake kuchukuliwa na Miraji Athuman.

Haruna Niyonzima

Simba itamkosa Morrison ambaye anatumikia adhabu ya kufungiwa mitatu, huku Kagere  na Gerson Fraga wakiwa majeruhi baada ya kuumia katika michezo iliyopita.

Kocha Mkuu wa Simba, Seven Vandenbroeck akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa tarehe 6 Novemba 2020 amesema, katika mchezo wa kesho Chama hatakuwemo kwenye mipango yake.

Wakati  Seven akiwakosa nyota wake hao ambao wamekuwa tegemeo katika kikosi cha kwanza, Kocha Mkuu wa Yanga, Cedric Kaze amesema, yeye atawakosa nyota wake Haruna Niyonzima anasumbuliwa na malaria, Mapinduzi Balama na Carlos Fernandes ‘Carlinhos’ ambao ni majeruhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!