Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Chama cha wapangaji waibua madai mapya
Habari Mchanganyiko

Chama cha wapangaji waibua madai mapya

Ndumey Mukama, Katibu mkuu  wa chama cha wapangaji
Spread the love

CHAMA cha Wapangaji   Tanzania (Tanzania Tenants Association), kimeiomba serikali kuweka chombo maalum kwa ajili ya kulinda maslahi ya wapangaji, anaandikaCatherine Kayombo.

Akizungumza na wanahabari, katibu mkuu  wa chama hicho, Ndumey Mukama amesema kuwepo kwa chombo hicho kutasaidia kusimamia sheria ya upangaji nchini ikiwemo ulipaji wa kodi kulingana na mandhari na hadhi ya nyumba husika.

“Kuwepo kwa mamlaka hii kutasaidia kusimamia na kuhakikisha kuwa hakuna mabadiliko ya viwango vya kodi za pango yasiyozingatia hali ya nyumba ya eneo husika na mwenendo wa soko” ,amesema Ndumey.

Katibu mkuu huyo pia ametoa rai kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi kuweka sera ya nyumba ili kusaidia kutoa mwongozo wa mwenendo wa suala la upangaji na kuweka mkakati utakaosimamiwa na serikali.

Aidha, uongozi huo umetaka udalali wa shughuli za upangishaji uzuiwe kisheria, na kutaka chama kipewe ridhaa ya kufanya hivyo kupitia chama chao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!