Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yatinga Ulaya kudai katiba mpya, tume huru 
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatinga Ulaya kudai katiba mpya, tume huru 

Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kinafanya ziara barani Ulaya kwa ajili ya kutafuta uungwaji mkono na Jumuiya za Kimataifa katika msuala ya uimarishaji demokrasia nchini, upatikanaji katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itifaki na Mambo ya Nje Chadema, John Mrema iliyotolewa Jana Jumamosi, ujumbe wa Chadema katika ziara hiyo unaongozwa na Makamu wake Mwenyekiti Bara, Tundu Lissu, wengine ni Katibu Mkuu, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalim.

“Ziara hiyo inahusisha nchi za Ujerumani na Ubelgiji ambapo ujumbe wa Chadema utawasilisha wito wa kuungwa mkono mpango wa kupatikana Kwa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, urudishwaji wa haki ya kufanya siasa ikiwemo mikutano ya hadhara,” imesema taarifa ya Mrema.

Taarifa ya Mrema imetaja taasisi ambazo ujumbe wa Chadema utawasilisha wito huo, ikiwemo Chama cha CDU, Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Ushirikiano was Kiuchumi na Maendeleo Ujerumani, Bunge la Umoja wa Ulaya na Taasisi ya Kimataifa ya Haki za Binadamu.

“Lengo ni kuhakikisha mazingira ya siasa Tanzania yanaimarika na katiba mpya na tume huru ya uchaguzi zinapatikana kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 Ili kuhakikisha uwepo wa uchaguzi huru, haki na unaokubalika,” imesema taarifa ya Mrema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!