Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yatimua wafuasi wengine wa Mdee
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatimua wafuasi wengine wa Mdee

Spread the love

 

WANACHAMA saba wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mkoani Mara wamevuliwa uanachama huku watatu wakiwekwa chini ya uangalizi kwa muda wa mwaka mmoja, kwa tuhuma za usaliti. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Jumatano tarehe 10 Machi 2021 na Lucas Ngoto, Mwenyekiti wa Chadema mkoani Mara, wakati anazungumza na wanahabari mkoani humo.

Wanachama hao waliofukuzwa Chadema ni, aliyekuwa Katibu wa Chadema Jimbo la Tarime Mjini, Peter Magwi, Jacob Kenyanga (Mwenyekiti Baraza la Wazee Chadema Wilaya ya Tarime) na Tecla Johannes.

Wengine ni, Sabato Amosi, Samwli Okendo, Paul Mwita na Isaya Mwita.

Waliopewa onyo na kuwekwa chini ya uangalizi ni, Steven Matiko. Richard Choge, Katibu wa Chadema Wilaya ya Butiama na Farajani Marwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), wilaya ya Butiama.

Ngoto alisema, wanachama hao wamefukuzwa Chadema, kwa tuhuma za usaliti kufuatia hatua yao kukaidi agizo la chama hicho la kutowatambua wabunge 19 wa viti maalumu, waliovuliwa uanachama.

Alisema wanachama hao, walikisaliti chama hicho kutokana na kuwaunga mkono wabunge hao kwa kuwasindikiza bungeni mjini Dodoma, hasa Ester Matiko, aliyekuwa Mbunge wa Tarime Mjini kupitia Chadema.

Mbali na Matiko, wabunge viti maalumu wengine waliofukuzwa Chadema ni, Nusrat Hanje, Halima Mdee, Esther Bulaya, Agnesta Lambart, Hawa Mwaigfunga , Grace Tendega, Jesca Kishoa na Tunza Malapo.

Wengine ni, Cecilia Pareso, Asia Mwadin, Felister Njau, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Stella Siyao, Salome Makamba, Anatropia Theonest na Conchesta Lwamlaza.

“Wengi katika kwenda Dodoma, wameupinga msimamo wa chama hadharani, sababu chama kupitia kamati kuu kimewavua uanachama waliokuwa wanachama wetu, kitendo cha wao kwenda kuwaunga mkono bungeni maana yake wameupinga ule msimamo wa chama hadharani na hilo ni kosa la kimaadili,” alisema Ngoto.

Ngoto alisema “kwa kukaidi na kwa sababu wanazozijua wao baadhi ya viongozi wa Jimbo la Tarime Mjini wameratibu zoezi hilo, na walienda safari hiyo pamoja na wanachama wetu na mwisho wake waliingia bungeni na wakatambulishwa kama wageni wa Matiko.”

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema

Ngoto alidai kuwa, kabla ya wanachama hao kutenda kosa hilo, walipewa onyo la kutoshirikiana na wabunge hao.

“Mwanzoni mwa Januari 2021 tulianza kupata taarifa kwamba baadhi ya viongozi na wanachama Mara wanaratibu zoezi la wanachama wetu kwenda Dodoma, kuwasindikiza ambao wamefukuzwa siku ambayo wanahudhuria bungeni mara ya kwanza,

“Sisi kama baraza la uongozi mkoa tuliitisha kikao, tulikubaliana tuwape tahadhari na kuzuia wanaoratibu zoezi wasishiriki safari hiyo sababu itakuwa inakiuka miiko ya chama chetu,”alisema Ngoto.

Wabunge hao 19 wa viti maalumu walifukuzwa Chadema tarehe 27 Novemba 2020, kwa tuhuma za kukiuka maagizo ya chama hicho ya kutopeleka wawakilishi wake bungeni, wakipinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

Wanachama hao walikuka maagizo hayo baada ya kukubali uteuzi wa ubunge viti maalumu, ambapo waliapishwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, tarehe 24 Novemba 2020.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!