Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yapinga msimamo wa Baraza la Vyama
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yapinga msimamo wa Baraza la Vyama

John Mnyika
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimekosoa msimamo wa Baraza la Vyama vya Siasa wa kuipa muda Serikali katika mchakato wa marekebisho ya Katiba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).

Msimamo huo umetolewa leo tarehe 15 Septemba 2023 na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akiwasilisha tamko la chama hicho kuhusu maadhimisho ya siku ya demokrasia duniani.
“Umma usikubaliane na maazimio ya mkutano wa baraza wa tarehe 13 Septemba 2023 ya kukwepa mahitaji ya haraka ya marekebisho ya Katiba ya 1977 katika Ibara zitakazowezwaha chaguzi huru na haki 2024 na 2025.

Aidha, usikubaliane na azimio la kuipa muda Serikali kuendelea kutathikini iwapo uchaguzi wa Serikali za mitaa uendelee kusimamiwa na TAMISEMI kupitia kanuni za Waziri au tume ya uchaguzi,” imesema taarifa ya Mnyika.

Mnyika amesema Serikali inatakiwa kupeleka bungeni muswada wa marekebisho ya Katiba ya 1977 kwenye mkutano ujao wa Bunge wa Oktoba 2023, kuwezesha chaguzi huru na haki, pamoja na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 kusimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

“Kwa tafsiri nyepesi demokrasia ni mamlaka ya watu na uchaguzi ni mamlaka ya watu kuweka watu wa kuwaongoza. Hivyo itakuwa ni unafiki kijivunia uwepo wa demokrasia nchini ikiwa wananchi hawana nguvu na mamlaka ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa uhuru, haki na uadilifu,” Amesema Mnyika.

Katika hatua nyingine, Mnyika amewataka vijana kushiriki shughuli za demokrasia na siasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!