CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinaugulia maumivu baada ya mwenyekiti wake katika Mkoa wa Njombe, Edwin Swale kutimkia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Tukio la Swale kuhamia CCM limefanyika tarehe 6 Oktoba 2019, katika ofisi chama hicho Wilaya ya Njombe ambapo mwanachama huyo mpya amekabidhiwa kadi.
Wakati akitimkia CCM, Swale amedai kwamba amevutia na kazi zinazofanywa na Rais John Magufuli hivyo amwekenda CCM kuungana naye.
Mwanachama huyo mpya wa CCM, mwaka 2015 aliwahi kugombea ubunge katika Jimbo la Lupembe kupitia Chadema
Leave a comment