Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yakomaa Umeya wa Jiji Dar, serikali yasalimu amri
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yakomaa Umeya wa Jiji Dar, serikali yasalimu amri

Spread the love

VUTA nikuvute kwenye Uchaguzi wa Naibu Meya wa jiji la Dar es salaam jana imesababisha serikali kuahirisha uchaguzi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tarehe ya uchaguzi huo itatangazwa baadaye baada ya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na yule wa Ubungo, Saed Kubenea kuapa kutodhuliwa.

Kilichosababisha vuta nikivute kwenye uchaguzi huo kwa baadhi ya vipengele vilivuoonekana kuwa n maslahi kwa upande mmoja.

Moja ya vipengele hivyo ni kutokukubaliwa kwa hati ya mgombea wa nafasi hiyo aliyetokea (UKAWA) kupitia Chama Cha Wananchi (CUF).

Katika mkutano huo baadhi ya wajumbe akiwemo Mdee na Kubenea wakiingia kwenye malumbano ya maneno na Mkurugenzi wa Jiji, Sipora Riama kuhusu hati ya mgombea huyo.

“Tunaomba hoja iliyotolewa na mjumbe Ndugulile aipokee Mkurugenzi na aseme ameikubali ili twende mbele, mheshimiwa ndugulile tumuulize Mkurugenzi amekubali kuja na utaratibu mpya kwenye kikao kijacho”, alisema Kubenea.

“Kwanini unaingilia majukumu yangu, huyu naye ni (Meya wa jiji) ana maslahi hawezi kutoa miongozo, mimi nina wanasheria hapa, maafisa utumishi ili kusimamia uchaguzi na miongozo mimi ndo natoa”, alisema Sipora wakati akizungumza kwa sauti kwenye kikao hicho.

“Nimshukuru Mheshimiwa Ndugulile, kwa kuwa tumekubaliana kuhairisha kikao, naomba UKAWA kupitia chama cha wananchi CUF kipate haki yake ya kupata mgombea wake, tunaomba kikao kinachokuja ajenda moja wapo iwe ni uchaguzi”, alisema Mdee kwa kumalizia.

Awali Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile alitoa ushauri wa kuhairishwa kwa ajenda ya uchaguzi kwenye kikao hicho, hoja ambayo ilikuja kukubaliwa mwishoni mwa kikao.

“Kikao chetu kimedumu kwa zaidi ya saa 4 kitu ambacho nakiona hapa, mjadala huu hautafika mwisho, naomba tuhairishe ajenda ya uchaguzi mpaka siku nyingine”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!