
Katibu wa Chadema Mkoa wa Morogoro, Samwel Kitwika
WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikiwa katika mchakato wa kutoa fomu kwa wagombea udiwani, ubunge na urais, mkoani Morogoro, watia nia wameanza kuitia hofu CCM. Anaandika Bryceson Mathias … (endelea).
Hivi karibuni, akiwa mkoani Mwanza katika ziara za kuimarisha chama, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, aliwataka wanachama wao wanaotaka kuwania uongozi huo, wajielekeze zaidi katika maeneo ambayo hawana wawakilishi kwa sasa.
Mkoani Morogoro agizo hilo limeanza kutekelezwa kwa kishindo. Akizungumza na MwanaHALISIOnline, Katibu wa Chadema mkoa, Samwel Kitwika amesema, majimbo yote 10 yamevamiwa na watia nia wa Chadema.
Pia, Kitwika amesema kuwa kata 212 za Morogoro, ziko kwenye mtikisiko, ambapo watia nia wanajitokeza kwa wingi kuchukua fomu.
Kitwika alibainisha idadi ya watia nia waliojitokeza hadi sasa na majimbo yao kwenye mabano kuwa ni 11 (Kilombero), 4 (Mikumi), 5 (Kilosa Kati), 3 (Gairo), 4 (Mvomero), na 7 (Manispaa ya Morogoro).
“Morogoro Kusini Mashariki wako watatu, Ulanga Magharibi (7) na Ulanga Mashariki (2) na Ulanga Magharibi tuna asilimia 100 tutashinda,”amesema Kitwika.
More Stories
Chadema wamng’ang’ania Spika Tulia ajiuzulu
Viongozi CHASO wataja sababu za kuikacha kuhamia ACT-Wazalendo
LHRC yataja mwarobaini changamoto mchakato wa katiba kuvurugwa na wanasiasa