Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaikaba Serikali mapato ya madini, yataka ripoti ya miaka 20
Habari za Siasa

Chadema yaikaba Serikali mapato ya madini, yataka ripoti ya miaka 20

John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema
Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitaka Serikali itoe ripoti ya mapato na matumizi ya fedha zilizotokana na madini yaliyochimbwa katika kipindi cha miaka 20 mfululizo, ili wananchi wajue wamenufaikaje na rasilimali hiyo. Anaripoti mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 23 Januari 2023 na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Tarime Mjini, mkoani Mara.

“Tarime uchumi wake unategemea madini, kunapaswa kuwe na mikakati ya dharura, moja Serikali itoe ripoti ya miaka 20 ya uchimbaji katika Mgodi wa North Mara, mapato kiasi gani yametumika, wananchi wamenufaika namna gani,”

“Pili, Serikali ieleze ukweli wananchi ni lini mapato yatasimama kwa sababu ya kuisha kwa dhahabu, tatu Serikali iwaambie Tarime mazingira gani inaweka kwa kushirikiana na sekta binafsi kuwa na uchumi mbadala baada ya madini kuisha,” amesema Mnyika.

Katika hatua nyingine, Mnyika amewataka wananchi wa Mara kupigania ajenda ya upatikanaji wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, ili kupata Serikali inayotatua changamoto zao.

“Taifa letu linahitaji katiba na tume huru ya uchaguzi, Mwenyekiti Mbowe ametuongoza kwenye mazungumzo ya maridhiano hatimaye uhuru wa kisiasa wa kufanya mikutano ya hadhara umefunguliwa, uhuru huu ni hatua moja ya ushindi lakini hatua kubwa tunayopaswa kupigania na kukamilisha ni mchakato wa katiba ili kabla ya 2025 Tanzania iwe na katiba mpya,” amesema Mnyika.

Katibu Mkuu huyo wa Chadema amesema kuwa, katiba mpya itakapopatikana itasaidia wananchi kupata viongozi wenye sifa ambao watasaidia kulinda maslahi yao na ya nchi kwa ujumla.

2 Comments

  • Katiba mpya ni muhimu sana wakati huu! Je kama watanzania tumejiuliza vitu,mambo muhimu yanayoitajika kuwemo ndani ya katiba yetu mpya?-katiba ni dira,muongozo usichezewe-kisiasa,binafsi,kidini! Tulijue hilo oou…!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!